Ray C afunguka kuhusu kuibiwa kwa ukurasa wake wa Instagram

Ray C amepoteza ukurasa wake wa Instagram uliokuwa na wafuasi zaidi ya laki tano. Mrembo huyo amefunguka na kusema kuwa akimpata aliyehack account yake atakipata cha mtema kuni.

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa radio, Ray C alieleza kukerwa kwake na aliyehack ukurasa wake wa Instagram.

download latest music    

“Mwizi aliyedukua (hack) akaunti yangu amenirudisha sana nyuma kwani nimeshindwa kufanya matangazo ya video ya wimbo wangu, matokeo yake nimetumia nguvu kubwa sana nilipouachia. Nikimkamata huyo mtu aliyenifanyia hivyo cha kwanza nitamnasa kofi kwa kunipa kazi cha pili lazima nimfikishe polisi na mwisho wake ni Segerea. Siwezi kuendelea kuvumilia watuibie halafu waendelee kukaa mitaani kwani watatutesa sana.

“Mimi akaunti yangu haijapotea kabisa kwani naiona ikiweka matangazo mbalimbali yaani nikimkamata sitamwambia anipe asilimia kumi bali atatoa pesa yote kwani nitahesababu tangazo la kwanza mpaka la mwisho ili kujua ni kiasi gani cha pesa anatakiwa anipe maana wameshazoea,” Ray C alisema.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere