Rayvanny Asitisha Ushindani Wa Kimavazi na Wasanii Wenzake

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka. WCB Rayvanny anayefanya vizuri na kibao chake cha ‘Chombo’ ameibuka na kutangaza Kumaliza ushindani wake wa kimavazi na wasanii wenzake huku akitaoa yeye ndio mshindi.

Sakata hili lilianza baada ya Dogo Janja kumtaja Rayvanny kama mmoja wa wasanii ambao haelewi anavaaga nini kwani hajui kujipangilia na kupendeza kitendo kilichomkera Rayvanny.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Dizzim Online, Rayvanny amesema kuwa anaamini ushindani upande wa mavazi anabaki kuwa yeye ni mwenye ujuzi na yuko katika viwango vya kuvaa vitu vya gharama zaidi hivyo hahitaji tena kushindana.

Akizungumzia hatua ya kutotaka tena kujihusisha na ushindani wa mavazi, Rayvanny aliongeza kuwa kwa sasa ana mambo mengi ya maana ya kufanya ikiwemo kujikuza zaidi kimuziki na kuandaa maisha mazuri ya mwanae JayDan kwa sasa na siku za Usoni.

Rayvanny ameendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Chombo’ ambapo ametangaza ujio wa video siku yoyote kuanzia hivi sasa.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.