Rich Mavoko Afunguka Baada Ya Kuwaburuza WCB BASATA

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Rich Mavoko amefunguka kwa mara ya kwanza na kuongelea sakata lake na uongozi wake wa zamani WCB.

Siku ya jana taarifa zilisambaa kuwa Rich Mavoko amepeleka kesi yake mbele ya Baraza la Sanaa (BASATA) baada ya Tetesi za wiki kadhaa kuwa ameamua kujitoa WCB.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rich Mavoko amesema kuwa anashukuru kukutana na BASATA na kupata elimu ya kutosha huku akiwamwagia sifa kuwa hao ndio maana halisi ya walezi wa sanaa yetu nchini Tanzania.

https://www.instagram.com/p/BmRCQzVAj05/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=133n0dixilgpb

Siku ya jana Rich Mavoko alikutana na Mkurugenzi Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza ambapo amepeleka mkataba wake na WCB ambapo ameomba uangaliwe upya na kudai ni wa unyonyaji.

Wasanii kadhaa na wafanyakazi wanaojitoa WCB wamekuwa wakilalamikia suala la mikataba mibovu kutoka katika kampuni hiyo na wengine kudai walikuwa hawalipwi.

Mpaka sasa uongozi wa WCB hawajajibu tuhuma hizo na madai hayo ya Rich Mavoko.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.