Rich Mavoko Amkana Lulu Diva Hadharani

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka kundi kubwa kabisa la WCB, Rich Mavoko amemkana hadharani msanii mwenzake Lulu Diva anayedaiwa kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na tetesi nyingi kuwa Rich Mavoko ana uhusiano wa kimapenzi na Lulu Diva ingawa wote wawili wamekuwa wakikataa tuhuma hizo na mara kwa mara Rich Mavoko amekuwa akigoma kuongelea suala hilo.

download latest music    

Wiki chache zilizopita habari zilienea kuwa Lulu Diva ametemwa na mwanaume anayejulikana kama Richard ambaye alikuwa mpenzi wake kwa kile kilichodaiwa kuwa aligundua kuwa Lulu Diva ana mchepuko ambaye ni Rich Mavoko jambo lilipopelekea kuvunjika kwa Mahusiano yao.

Lakini pia ilidaiwa Lulu Diva alinyang’anywa kila kitu alichopewa na mpenzi wake huyo baada ya habari hizi kusambaa kwa kipindi kirefu Rich Mavoko hatimaye amefunguka kwenye interview na Lemutuz Online na kumkana hadharani mchana kweupe Lulu Diva:

Lulu Diva kwangu ni mtu wa kawaida tu kama watu wengine yaani ni rafiki yangu kama marafiki wengine wa kawaida sina uhusiano naye mwingine zaidi ya huo”.

Rich Mavoko pia amewataka mashabiki zake wakae mkao wa kula kwani anapika nyimbo zake mpya jokoni kwa hivi sasa na angependa wasikilize muda ukifika.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.