Roma Amuanika Mtoto Hadharani Kwa Mara Ya Kwanza

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kuchana Ibrahim Musa maarufu kama Roma Mkatoliki amemuweka mtoto wake hadharani kwa mara ya kwanza tangu azaliwe Miezi michache iliyopita.

Roma na mke wake Nancy walijaliwa kupata mtoto wao huyo wa Pili ambaye ni wa kike ambaye anaitwa Ivy lakini kutoka na ukimya wao mtoto huyo hajawahi kuonekana Kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

BAADA ya kumficha kwa kipindi cha miezi sita, Roma Mkatoliki’ ameamua kumuanika mwanaye wa kike, Ivy. Ishu hiyo imetokea juzikati, baada ya Star Showbiz kumtimbia nyumbani kwake, Mbezi- Jogoo jijini Dar ambapo alikuwa akifanya sherehe ya kumbatiza mtoto huyo.

Nimekuwa siyo mtu wa kuanika anika hovyo maisha yangu na wanangu lakini kwa kuwa umetokea haina jinsi, huyu hapa ni Ivy, leo ndiyo amebatizwa rasmi“.

Msanii huyo ambaye Yupo Kwenye kikundi na msanii mwenzake Stamina ‘Rostam’ wanafanya vyema na ngoma yao ya Parapanda.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.