Sababu Za Lulu Kutokuwepo Katika Msamaha Wa JPM Zatajwa.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Juma Malewa amefunguka sababu za Lulu Michal  kutokuwepo katika listi ya majina ya wafugwa waliopewa msamaha wa Mh.rais tarehe 9 December mwaka huu kama vile ambavyo watu wengi walivohisi  itakuwa.Lulu  alianza kifungo chake November mwaka huu baada ya kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia.

Mapema mwaka huu Mh.Rais alitoa tamko la kuwasamehe wafungwa  kwa vigezo mbalimbali huku mashabiki wa msanii Lulu Michael wakiwa na matumain ya kumuona msanii wao akiwa katika moja ya wafungwa watakao pewa msamaha huu kwa sababu wasanii wengine wakongwe walipewa msamaha huo.Hata hivyo kamishna huyo alisema kuwa lulu michael aliingia gerezani kipindi ambacho mchakato wa kutafuta wafungwa wa kupewa msamaha wa Raisi ukiwa tayari ulishaaanza hivyo isingekuwa raisi kuwekwa katika list hio kama watu wanavyofikiria.

download latest music    

Msamaha huu haukumuhusu kwa sababu kipindi anaingia magereza mchakato wa kupata wafungwa wa kupewa msamaha tayari ulikuwa  umeshaisha.Kwaio labda misamaha mingine ijayo kama itakuwepo  lakini huu haukumuhusu kabisa.

Hata hivyo Kamishna Malewa amesema kuwa kuna vigezo vingi ambavyo huwa vinaangaliwa mpaka mfungwa kupewa msamaha au kupunguziwa kifungo chake, kwa kuangalia muda wa kifungo chake na kosa lake pia na jinsi hukumu ilivyotoka , lakini pia wanaangalia jinsi mfungwa anavyokuwa anafuata masharti ya kifungo chake na jinsi gani kifungo hicho kimeweza kumfunza kitu.

Baada ya Mh. Rais kutoa msamaha kwa watu wnegi ikiwepo Babu Seya na Nguza Viking mashabiki walianza kuhoji kwanini Lulu Michael hakuhusishwa katika msamaha huo, lakini Kamishina ameona bora kufunguka na kuelezea kwa undani swala hilo.

Lulu Michael amepewa kifungo cha miaka miwili baada ya kukutwa na hatia ya kumuua Kanumba Steven aliyekuwa mpenzi wake baada ya kuwa na ugomvi uliosemekana kuwa ni wa wivu wa mapenzi.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.