Saida Karoli: Watu wameanza kutumia ushirikina kunipiga vita

Saida Karoli amekiri wazi kuwa suala la ushirikiana lipo na kwake si jambo la ajabu. Muimbaji huyo amedai kuwa kuna baadhi ya watu ambao wanatumia ushirikina kumpiga vita ili aweze kupotea tena kwenye muziki kama ilivyotokea kipindi cha nyuma.

Karoli alifunguka na kusema kuwa kuna mtu ambaye alilipwa pesa ili amuuwe kabisa, jambo ambalo lilimlazimisha yeye kuahirisha baadhi ya show zake.

download latest music    

“Huyo mtu alinielekeza watu kadhaa ambao wamepanga mpango wa kuniua aliniambia, sasa mimi nimeshalipwa nikuuwe nikuondoe duniani kabisa yaani kabla ya kufika Mwanza, Geita tena bora hata hizi show zingine uvunje, kweli ramani aliyonipa nilichoka ikabidi show zingine za Bukoba tumezivunja tukasema ngoja tutulie kwanza tuone nini kitaendelea” alisema Said Karoli

Saida Karoli anadai kurejea kwake kwa muziki kumewakera watu wengine ambao wanataka kumua. Staa huyo ambaye kwa sasa anawika kwa wimbo wake mpya ‘Orugambo’ ata hivyo alisisitiza kuwa yeye anamtegemea Mungu tu.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere