Sheikh Kipozeo Amwaga Povu Baada Ya Diamond Kuonekana Kavaa Kikuku

Sheikh Kipozeo ambaye amekuwa akitoa mawaidha katika mambo ya maadili, amefunguka ishu ya wanaume kuvaa cheni miguu ambapo amedai wanaume wanaojifanisha na wanawake kwa kuvaa cheni wamelaaniwa na Mwenyezi Mungu.

Wikiend iliyopita Diamond alizua gumzo Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana akiwa amevaa cheni ya mguuni ‘kikuku’ ambacho mara nyingi kinavaliwa na wanawake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Sheikh Kipozeo amefunguka na kusema sio kwa Diamond tu wanaume hawaruhusiwi kuvaa vitu ambavyo vinavaliwa na wanawake.

Mwanaume harusiwi kuvaa cheni halafu sio miguuni tu hata shingoni haruhusiwi kwa sababu cheni ni pambo la kike na Mungu amewalaani wanaume wanaojifananisha na wanawake na wanawake wanaojifanisha na wanaume.

Mtu yoyote tu mwanaume sio Diamond peke yake atakayevaa vazi la kike basi atalaaniwa na Mwenyezi Mungu”.

Kwa maadili ya Kiafrika cheni ya mguu yaani kikuku kimekuwa kikivaliwa na wanawake lakini kwa nchi za wenzetu ni jambo la kawaida kwa wanaume kuvaa wasanii wakubwa kama Chris Brown wameonekana wamevaa vikuku.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.