Shekhe Amjia Juu Diamond Kwa Mavazi Ya Tanasha

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, Amemjia juu  mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, kwa mavazi ya mpenzi wake Tanasha.

Gazeti la Risasi linaripoti kuwa Tanasha alizua gumzo wiki iliyopita Baada ya kuonekana akiwa amevaa gauni ambalo liliweka sehemu kubwa ya maungo yake nje jambo ambalo pia limeonekana kumkereketa Shehe mkuu.

download latest music    

Jamani…jamani…ndiyo nguo gani ile mbele ya kiongozi wa dini? Kiukweli si sawa na ndiyo maana hata Shehe Alhad alikataa kumpa mkono Tanasha na kuishia kumpungia. “Kwani Tanasha hakujua au hakuambiwa anakwenda kwenye mkusanyiko wa watu wengi wa kada mbalimbali ili ajisitiri? Ona sasa anavyoaibika hata anashindwa kutazama watu kutokana na aibu.

Lakini yote kwa yote, wa kulaumiwa hapa ni Diamond kwani ndiye aliyetakiwa kumpanga mtu wake juu ya namna ya kuvaa kwenye shughuli kama hii. Kiukweli atakuwa amemtibua mno Shehe Alhad”.

alisema mmoja wa wahudhuriaji waliokuwa wamedamshi ile mbaya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Mchanganyiko juu ya kitendo hicho na kwamba alikichukuliaje, Shehe Alhad alitema nyongo kwa kumvaa Mondi mzimamzima.

Diamond hakufanya kitu kizuri, lakini alitekeleza amri ya Mkuu wa Mkoa wa Dar (Paul Makonda) kujitokeza pale mbele na mwenzake (Tanasha).

Lakini hata mimi nilivyokwenda pale mbele sikupendezwa kumuona huyo mwanamke na ndiyo maana hata hukuniona nikimpa mkono wangu. “Ila niliheshimu kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa kumpa mkono Diamond, lakini yeye (Tanasha) sikumpa mkono kwa kuwa nilimuona yupo vile.

Lakini pia Diamond naye anaonesha udhaifu kwa mwanamke kwa kumuacha namna ile kwa sababu mali zako lazima uzione wewe mwenyewe, mwanaume lazima uwe na wivu, haiwezekani unayetarajia kumuoa mwili wake unakuwa wazi ina maana hana thamani. “Diamond anatakiwa kumuongoza yule binti (Tanasha), hakutakiwa kumuacha vile.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.