Shetta Athibitisha Kuwa Utovu Wa Nidhamu Wamfukuzisha Ruby ‘King Empire’

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Shetta ambaye pia ni mmoja wa viongozi Katika kampuni na Recording Label ya Kings Empire ameweka wazi sababu za kusimamishwa Msanii Ruby.

Kings Empire inasimamia wasanii Kama vile The Mafik, Aslay na wengineo wameweka wazi mmoja wa aliyekuwa Msanii wao Ruby hayupo tena na Label hiyo kutokana na kukosa nidhamu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Clouds FM, Shetta ameweka wazi kuwa  Ruby alisimamishwa na label hiyo baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu.

Siwezi kusema sababu bali sisi ni familia kuna vitu vinatokea hata wachawi hugombana usiku wakiwanga, Hivyo kulitokea mpishano wa kauli kati yake na Meneja Kapasta kwenye group hivyo nikamwambia Ruby muheshimu kiongozi mara akanivamia na mimi hivyo nikamwambia #hambuso aandike barua ya kumsimamisha kwa muda kwa utovu wa nidhamu na angerudi tungezungumza lakini naona akaamua kufanya kazi zake yeye kama yeye“.

Skendo ya kuwa na kiburi na jeuri imekuwa ikimuandama Ruby kwa muda sasa ambapo watu kadhaa aliofanya nao kazi wameshawahi kumtuhumu kwa kuwa na tabia hizo ingawa mwenyewe ameshawahi kukataa taarifa hizo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.