Shilole Amtema Zari na Kumkubali Tanasha

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amedaiwa kumsaliti na kumwaga Zari na kumkubali zaidi Mpenzi Mpya wa Diamond Tanasha.

Kama utakumbuka siku mbili zilizopita Shilole alisimama mbele ya waandishi wa habari na kumuomba Diamond aachane na Tanasha na kumuoa mama Watoto Wake Zari.

download latest music    

Lakini sasa Shilole ameonekana kukubaliana na hali halisi na kumkubali Tanasha kama wifi yake mpya na kusema wazi kuwa anapopenda Diamond basi na yeye hana budi kufuata.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shilole ameandika maneno haya:

ANAPOPENDA KAKA YANGU SINA JINSI! HI TANASHA, DIAMOND PLATNUMZ WIFI YETU KARIBU DADA HII NDO TANZANIA NITAFANYAJE SASA JAMANI”.

Ni takribani mwaka mmoja tangu Diamond kuachana na Zari na kuanzisha mahusiano mapya na mrembo Natasha kutoka nchini Kenya. Hivi karibuni Diamond Platnumz alikaririwa na kituo hicho cha runinga akieleza kuwa ndoa yake aliyopanga kuifunga mwezi wa pili mwaka huu ameisogeza mbele.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.