Shilole awatolea povu mashabiki zake

Shilole amekasirishwa na baadhi ya mashabiki wake wanaodai kuwa yeye bila ya kiki na kukaa mtupu hawezi kufanya vizuri katika kazi zake za kimuziki.

Hii ni baada ya mrembo huyo kuachia wimbo mpya ‘Kigori’ ambayo mbaka kwa sasa haijafanya vizuri katika mitandao ya kijamii.

download latest music    

Akiongea katika kipindi cha Friday Night Live ‘FNL’ cha EATV, Shilole alieleza kuwa wimbo wake haujafanya vizuri kutokana na yeye kutokata viuno kama mashabiki zake walivyozea kumuona katika nyimbo zake za awali alizowahi kufanya.

“Sikutaka skendo katika hii video, nilitaka kuwachukua wale real mashabiki zangu, nimefanya video nzuri kama mtoto wa kitanzania yenye maadili mazuri kwa ajili ya kila mtu, sijakaa utupu kabisa kwenye ‘video’ hii kama watu walivyozoea. Kwa hiyo inabidi tuwabadilishe na ndugu zetu watanzania waweze kuelewa kuwa kuna ‘video’ hii inataka iwe hivi na nyimbo hii inataka hivi ‘so’ kuna nyimbo za matashititi. Tuanze kukubali muziki kwanza siyo lazima kila siku niwe Shilole wa fujo fujo tu“, alisema Shilole.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere