Shilole na Uchebe Wamefungukia Tetesi za Kuachana

Mume wa Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole, Uchebe amefunguka kuhusiana tetesi zilizoiandama ndoa yao mwanzoni mwa wiki hii ambapo ilisemekana kuwa wameachana.

Tetesi hizo ziliwashwa pale ambapo Uchebe aliweka UA jeusi kwenye ukurasa wake wa Instagram kuashiria penzi limeingia shubiri na baadae Shilole alilalamika kwenye redio kuwa Uchebe amempa kipigo cha mbwa mwizi.

download latest music    

Alipohojiwa mwandishi kutoka East Africa Tv, Shilole alikana tuhuma zote hizo na kusisitiza kuwa hajaachana na mume wake na wala hana mpango wa kufanya hivyo kwa muda wowote kuanzia sasa.

Lakini na Uchebe nae amesisitiza kuwa hajaachana na mke wake bali kuna watu ambao wanafiki hawataki kuwaona wakiwa wote na nia yao kubwa na kuwagombanisha ili waachane.

Uchebe alipoulizwa kuhusiana na lile Ua alilo liposti ambalo lilizua mambo yote hayo Uchebe alidai kuwa kuna mtu alimhack kwenye akaunti yake na kuuweka upuuzi ule.

Sio kweli sijaachana na mke wangu na wala hatufikirii kuachana, kuna watu wanafiki wanapenda kusikia tumeachana, kuhusu ile post kuna mtu alifanikiwa kuhack acount yangu na kupost vile lakini sijamuacha mke wangu, na wala hatuna ugomvi, na niwaambie tu kuwa hatuachani leo hata kiama”.

Wawili hao walifunga ndoa ya siri mwaka jana mwishoni lakini walikuja kuhalalisha kwa sherehe mapema mwaka huu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.