Sitaachika Kwa Mume Wangu Ng’oo-Shamsa Ford

Msanii wa filamu za Bongo Movie Shamsa Ford amefunguka na kuungelea tetesi zilizozuka wiki iliyopita kuwa yeye na mume wake mfanyabiashara Chid Mapenzi wameachana.

Tetesi za Shamsa na Chid kuachana ziianza baada ya Shamsa kuweka status iliyosomeka:

download latest music    

Mapenzi au kumpenda mtu, kusikufanye uwe mtumwa… ukiona unampenda mtu halafu anakuchukulia poa achana naye. Maisha ya sasa hivi, siyo ya kujipendekeza au kulazimishana… mtu uwaze maisha magumu bado mapenzi yakusumbue? Acha ujinga na usikubali kuwa mtumwa… wewe funika sura fanya kama huoni..”.

Kwenye mahojiano Gazeti la Risasi Jumamosi, Shamsa alisema kila akiweka ‘status’ kwenye ukurasa wake wa Instagram inayohusu ishu za kuachana, kuna wanaodhani inamhusu yeye, wakati huwa kuna ambao wamekuwa wakiomba ushauri na kwa sababu hawezi kumshauri kila mtu kwa wakati wake, huamua kuandika kwenye ukurasa wake.

Unajua nilipoweka ‘status’ kila mtu alinihoji na wengine kunifuata ‘DM’ wakitaka kujua nini kimenikuta, niwaambie tu kwamba sitaachika mpaka Mungu atakapotutenganisha ingawa wapo wanaoniombea hilo kila siku”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.