“Sitakubali Uchebe Aoe Mke Wa Pili”- Shilole

Msanii machachari kabisa wa Bongo fleva mwanadada Shilole amefunguka na kusema katu hatokaa akubali mume wake Uchebe aje aoe mke wa pili kwani yeye hana kasoro yoyote.

Siku chache zilizopita Mkuu wa wilaya ya Pangani, Tanga Bi. Zainab aliushangaza uma wa Watanzania na hata baadhi ya nchi za jirani kwa uamuzi wake wa kumruhusu mume wake aoe mke wa pili ili wasaidiane majukumu ya kumlea.

download latest music    

Baada ya sakata hilo kutrend vibaya mno kwenye mitandao ya kijamii Millard Ayo Tv ilimsaka msanii Shilole ili kumuuliza nini mtazamo wake juu ya jambo hilo kwani na yeye ni mwanamke wa kiislamu aliyeolewa na mwanaume wa kiislamu je kama ataweza kukubali Uchebe alete mke wa pili.

Kwenye Interview hiyo Shilole alifunguka haya yafuatayo:

Kwanza nikuweke wazi kabisa kuwa mimi mume wangu hawezi kuoa mke wa pili hata siku moja yaani hata kama dini inaruhusu unaoa mke wa pili ili iwaje yaani , kwanini? Yaani mimi nina  mapungufu gani mpaka ukaoe mke mwingine mtu mwingine ana mapungufu huwezi kujua lakini mimi sina mapungufu yoyote na mume wangu hawezi kuniacha na kuoa mke wa pili”.

Shilole amesisitiza wanaume wanaotaka kuoa wake wengi kibao hawaijui dini na wanaoa wake wengi kwa ulafi na tamaa lakini pia amesema endapo mume wake atataka mke mwingine basi atamuacha aoe kwa amani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.