Steve Nyerere Akiri Kuzichoka Sura za Bongo Movies.

Msanii mkongwe wa maigizo ya bongo movies ambae pia ni mshekeshaji maarufu bongo amekiri kuwa uweo wa wasanii walewale kila siku  kunafanya bongo movies ichokwe na kila mtu kwa sababu ladha ya maigizo inakuwa haibadiliki bali kila siku ni walewale.

Msanii huyo ambae ameluwa akipigania kuinuka kwa bingo movies kila siku anasema kuwa inabidi kuwepo na wasanii wapya ktaika tasnia ili kuleta ladha mpya ya uondo wa bongo movie lakini kitu cha ajabu hakuna wasanii wapya katika maigizo.

download latest music    

Akitolea mfano alipokuwa akiongea na  Ijumaa wikienda , Steve Nyerere anasema kuwa inawachosha watu wengi kama kila siku wanakuwa wakiona sura za Kajala Masanja , Shamsa Word au wolper kila siku  na ndipo linpotokea anguko la sinema za bongo kama ilivyotokea sasa hivi.

Akiendelea kuongezea Steve anasema kuwa ifike mahali wasanii wakubwa na wakongwe wabaki kupewa heshima yao kama wasanii wakongwe na kuwaibua wasanii wapya ili kuleta ladha tofauti na zile za zamani ili kuifanya tasnia kuwa na mabadiliko kidogo.

ninachokipigania mimi ni kuwa wasanii wasanii wakubwa wabaki kuwa na hati miliki zao,lakini sura za mastaa hao hao kila siku katika kioo zinachsha kabisa, maana hata mimi nimezichoka.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.