Steve Nyerere atoa ushauri wake kuhusu bifu mpya kati ya Diamond, Alikiba na Ommy Dimpoz

Diamond Platnuz, Alikiba na Ommy Dimpoz wamekua wakitupiana maneno yenye mafumbo katika mitandao ya kijamii tangu Diamond aliposhirikishwa katika remix ya ngoma ya Fid Q ‘Fresh’.

Diamond alisema kwa wimbo huo kuwa hawezi kulinganishwa na Alikiba kisha Kiba naye akamjibu kwa fumbo kuwa yeye bado ndo mfalme.

download latest music    

Diamond tena aliweka wimbi nyingine kwenye account yake ya Instagram ambayo aliwachimba Alikiba na Ommy Dimpoz. Baada ya Diamond kuweka wimbo huo kwa Instagram, Ommy Dimpoz pia aliweka picha Instagram akiwa na mama mzazi wa Diamond na kuandika ujumbe wenye utata:

Ommy Dimpoz na mamake Diamond

“BARUA YA WAZI KWA BINTI YANGU MALKIA WA NGUVU

Salam zako nimezipata mwanangu Hivi kweli ww wa kukosa Adabu na kuamua kunichamba mimi Baba yako? Sasa kosa langu mimi nini???? Kwani kuna Ubaya kumtandikia Kitanda Baby wako King?

#UnanioneaKwaKuaSijuiKurap?

#SijuiNaMimiNimkatae??

#KamaYeyeAlivyomkataaWaMobeto

#YaniUnamkataaMjukuuWangu??

#UnakubaliKuleaWatotoWa5SioWako

#UmerogwaWWSioBureMwanangu

#NilikuwaNajuaNimezaaSIMBA

#KumbeNimezaaKIMBA

#DavidoNaeAnalalamiKuhusuENEKA

#UmeletaJanjaJanjaKwenyeFallOnU

#NnaedhalilikaMimiBabaYaKo??

#UtakujaKuniuaKwaPreshaJomoniiii?

#HayaNendaKatungeVesiNyingine?

#RahaYaVitaUsichagueSilaha

#BABAMALKIA

 

Steve Nyerere sasa ameingilia kati na kutoa ushauri wake, somo ujuembe aliondika kwa Instagram hapoo chini:

“NIMEKAA NIMEJIFIKIRIA NIMEONA NISEME KIDOGO, DUNIA MAMA ANA HESHIMA YAKE KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE, MAMA NI KIOO CHA FAMILY MAMA NI NGUZO YA FAMILY MAMA NI KIMBILIO LA FAMILY , TUNAWEZA KUKOSEA KOTE LAKINI SI KWA MAMA NDOMANA AMNA LAANA YA BABA ILA LANA YA MAMA IPO NA INAFANYA KAZI HARAKA KULIKO KITU CHOCHOTE, SIZANI KAMA TUNA ELIMISHA JAMII KUPITIA MATUSI YA KUZALILISHA WAZAZI, NYINYI NI KIOO CHA JAMII, LAZIMA MUWE NA KIFUA CHA KUBAKISHA MANENO , MIMI NILIZANI HIZI NGUVU MNAZOTUMIA MNGEWEKEZA KWENYE MZIKI WENU TUNGEFIKA MBALI SANA , MMEJIJENGEA HESHIMA NA MMELITAFUTA JINA KWA SHIDA , ILA MNASAHAU JINA HILO LINAWEZA POTEA KWA SEKUNDE, NAWASHAULI NA NAKUSHAULI WEWE UNAYEZARAU WAZAZI FUTA KAULI NA OMBA MSAMAHA KWA MASHABIKI ZAKO USUSANI KINA MAMA WOTE AMBAO NAAMINI NI MASHABIKI WAKO NA NDIO WALIOKUFANYA UKAFIKA HAPO, HATUKATAI NYINYI NI BINADAMU INAWEZEKANA MMEPISHANA KAULI ILA KWENYE KUPISHANA WEKENI AKIBA YA MANENO, KUNA KESHO HUJUI ATAKAYE KUSTILI, HAKIKA BUSARA ITUMIKE , YANI NINGEKUWA MIMI NDIO UMEMGUSA RITA WANGU IVO DOOOO, MJINGA HAJIBIWI, KICHAA HAKIMBIZWI , MWIZI SI RAFIKI, NANI KAMA MAMA, ESHIMA ITAWALE ASANTE BY #####UZALENDO KWANZA.”

Steve Nyerere

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere