TID Afungukia Sekeseke La Kudhulumiwa Mtoto

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Khaleed Mohamed maarufu kama T.I.D amefunguka na kuweka wazi kuwa taarufa zinazosambazwa na mzazi mwenzake kuwa Mtoto sio Wake sio za kweli.

Mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la shekha ametengeneza headlines siku chache zilizopita baada ya kumkataa TID kama baba wa Mtoto Wake na kumtaka Msaniii kutoka Kenya Prezzo kama baba Watoto Wake.

download latest music    

Shekha amemtaka TID kukaa mbali naye na Mtoto Wake kwani anajua wazi kuwa yeye sio baba wa Mtoto huyo hivyo aendeleee na maisha yake na amuache yeye na Prezzo wamlee Mtoto wao.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, TID ameendelea kushikilia  msimamo wake kuwa mtoto huyo ni wake hata aje nani anachojua ndiyo hicho na si kitu kingine chochote.

Jamani hata aseme nini mtoto ni wa kwangu yeye ataongea mpaka basi lakini ajue mtoto ni wangu hata mtoto atakuwa anajua, huyo Shekha anajidanganya nafsi yake mwenyewe”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.