Tunda Amwita Petit Man Chawa Wa Wasafi

Mwanadada asiechuja ambae amekuwa akifanya vizuri mpaka sasa kutokana na kuuza sura katika video za wasanii mbalimbali ikiwemo video ya Diamond Platinumz  ‘Salome’, amemwita Petit Man mume halali wa Esma Platinumz kuwa ni chawa kutokana na kufatana fatana na Diamond na kundi la wasafi kila sehemu, ,Petit Man ni moja kati ya wanafamilia ya wasafi kwa sababu ni mume wa dada yake na Diamond anaejulikana kama Esma Platinumz.

Katika moja ya post katika kurasa za Dizzimonline, katika ukurasa wa instagram ambapo ilipostiwa picha ikimuonyesha Petit Man akiwa na mke wake Esma na Aunty Ezekiel akiwepo, Tunda alicoment na kumuita Petit Man kuwa ni chawa wa wasafi.

download latest music    

“Petiiman hatimaye amekuwa chawa wa WCB, kweli maisha yanabadilika” aliacha comment iyo katika picha, hata hivyo Petit Man na Tunda walikuwa wakionekana pamoja na hata kufanya kazi  pamoja lakini kinachshangaza mashabiki kuwa ni kwanini Tunda aandike ujumbe kama huo tena wazi katika post ambao watu wengi wangeiona au alijua kabisa kuwa lazima ujumbe utafika.

Hata hivyo , picha iyo ni moja ya picha zinazoonyesha matukio  na watu waliokuwa wameudhuria katika show mojawapo alioifanya Damond Platinumz  na Rayvanny katika uwanja wa Amani huko Zanzibar , Petit Man akiwa kama shemeji na mtu wa karibu wa familia ya Diamond alikuwepo kwa ajili ya kusapoti show hiyo.

Hata hivyo show iyo ilihudhuriwa na watu na wasanii wengi maarufu ikiwemo Aunty Ezekiel kutoka bongo movie, Zari The Bossy ambae baada ya kumaliza uzundizi wa  duka jipya Mlimani City mali ya Gsm waliondoka na kuelekea Zanzibar.

Hii sio mara ya kwanza kwa Petit Man na mkewe kutokea katika events na party za familai ya Diamond, na akiwa kama mwanafamilia na mtu anaesapoti sana muziki wa Tanzania basi anapotokea katika shughuli kama izo anakuwa pia na umuhimu wake kwa mkewe na kwa wasanii pia kwa sababu petit man alishawahi kuwa meneja wa wasanii mbalimbali wa bongo fleva na bado anaendelea kusapoti baadhi ya wasanii.

Tunda akiwa pamoja na Petit Man

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.