Ushauri Wa JB Kwa Wasanii Wenzake Wa Bongo Movie

Muigizaji wa Bongo movie Jacob Steven maarufu kama JB amewapa usia wasanii wenzake wa Bongo movie.

Miaka ya hivi karibuni soko la bongo movie limeshuka kwa kiasi fulani nikimaanisha ni tofauti na ilivyokuwa miaka michache ya nyuma huku watu wengi wakikosoa filamu hizo zinazotolewa na solo hilo huku wasanii wengi wakilaumu wizi wa kazi zao na bajeti finyu.

download latest music    

Wasanii wakongwe kama JB wamekuwa wakitafuta njia sahihi za kuweza kulikoa soko la Bongo movie, JB kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alifunguka yafuatayo;

“Kanuni za uvaaji zinasema kabla hujaambiwa hiyo nguo ni nzuri ni lazima wewe mwenyewe uipende ndio maana mtu akikuuliza kati ya nguo hizi ipi nivae ukichagua nyingine utasikia angalia vizuri hii anakuonyesha anayoitaka hata tukija kanuni za utongozaji zinasema lazima ujikubali mwenyewe ukijichukia yule unayemtaka atachukia zaidi mfano kama kazi yako ni kuzibua choo halafu ukamdanganya mtu wewe ni banker maana take umejichukia, Kwanini nimesema haya ukiangalia account za wasanii wengi wa filamu kwa mwezi mzima anaweza asipost kitu chochote kinachohusiana na filamu, najua wengi wenu ni vijana na ni wakati wenu na lazima mpost mambo yenu lakini nawakumbusha Fulani ndo ziliwafanya muitwe majina hayo”.

Pia JB aliendelea kufunguka kuwa;

“Mashabiki wanawafahamu kwa ajili ya movie tafadhali tusijisahau, walau kwa wiki mara mbili Mimi nimepunguza sana kupost mpira ni movie tu na nimeacha kuwafollow watu wasiohusiana na movie hata mke wangu, nyie msifanye hivyo kama mimi lakini naomba nione post za movie kwenu…tuamke tuzitangaze movie zetu”.

Je unahisi juhudi hizi zitatosha kuokoa soko hili la Bongo movie?

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.