Uwoya Afungukia Tetesi Za Kuiba Mume wa Mtu

Muigizaji wa Bongo movie nchini Irene Uwoya amefunguka na kuongelea skendo iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya kwamba yeye ameiba mume wa mtu.

Sakata hilo lilianza Wiki iliyopita Baada ya Uwoya kuposti picha akiwa na mwanaume mwingine huku akiwa amemziba uso na kusababisha kuzua maneno lakini mambo yalibadilika Baada ya picha za harusi za mwanaume huyo kusambaa akiwa na mke wake na kupelekea Uwoya kutuhumiwa kwa kuiba mume wa mtu.

download latest music    

Katika mahojiano yake na Gazeti la Ijumaa, Uwoya amewajia juu watu waliozusha skendo hiyo na kusema kuwa hawajui wanachokiongelea kwani mwanaume Yule aliyepiga naye picha ni mjomba ale kabisa.

Ndiyo maana siku zote mimi nawaambia watu waache unafiki maana wako macho kuona Irene (Uwoya) anaharibu, lakini wanashindwa kufuatilia ukweli wa jambo hilo hata kidogo tu.

Yule ni mjomba wangu kabisa jamani, inakuwaje anakuwa mwanaume wangu? Huko si ni kuvinjiana heshima? Tena kubwa na isitoshe mjomba wangu huyo alikuwa na mke wake, lakini kwa sababu watu wanapenda kufuatilia mambo, wakaibuka na hivyo”.

Lakini pia Uwoya amedai kwamba alivyoweka picha yake alijua tu yatatokea hayo ndio maana akaamua kumziba sura yake lakini bado watu walifokonyoa Mpaka wakamjua ni nani.

Nilijua tu ndiyo maana nikamziba sura, kuna wanafiki watajitokeza na kuyaleta yao, lakini kwa hapo wamefeli na tena kama ni mtihani wamepata F au ziro kabisa“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.