Uwoya Amwaga Povu Juu Ya Mahusiano Yake na Dogo Janja

Muigizaji wa Bongo movie Irene Uwoya amejikuta akimwaga povu zito baada ya kuhojiwa kuhusu Mahusiano Yake na mume wake staa wa Bongo fleva Dogo Janja.

Siku za hivi karibuni Kumekuwa na tetesi nyingi zinazoizunguka ndoa ya Uwoya na Dogo Janja ikiwemo kuwa wawili hao wameachana baada ya Wolper kupata mwanaume mwingine mwenye pesa zaidi anayemuweka Mjini kwa sasa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya Global Publishers hivi karibuni Uwoya alihojiwa juu ya taarifa za kumtesa Kimapenzi Dogo mpaka kuishia kulazwa hospitalini halafu inadaiwa hakuenda kabisa kumuona badala yake alidaiwa kuonekana batani.

Wolper alimwaga povu zito baada ya swali hilo:

Wanasema anaumwa kwa ajili yangu? Basi hayo makubwa! Sijawahi kusikia kuna ugonjwa wa mapenzi. Kwa hiyo ina maana mimi huwa ninawatesa watu? Mimi huwa siteswi? Maana kila mtu Uwoya… Uwoya…ina maana kila ishu ya mapenzi mimi ndiye huwa natesa watu? Kwa hiyo mimi ni tesatesa au chinjachinja wa mapenzi? Ni kweli mimi ni mkali, lakini huyo mwanaume atakuwa na ugonjwa mwingine siyo mimi”.

Lakini pia Uwoya alipoulizwa endapo tetesi za kuachana Dogo Janja mpaka kuishi nyumba tofauti ni za kweli alijibu:

No Coment! Kwani wakati tunaanza tuliwatangazia? Hilo waambie sina majibu, nimesema no coment!”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.