Vanessa Mdee: Mapenzi yangu na Jux hayakuwa ya kisela

Wiki mbili zimepita sasa tangu Vanessa Mdee kuachia wimbo wake mpya wa kimapenzi ‘Kisela’ aliyomshirikisha Peter Okoye wa P Square.

Mdee, ambaye aliwachana na mpenzi wake Juma Jux, alifunguka kuhusu uhusiano wake na mwanamuziki huyo.

download latest music    

Mrembo huyo alieleza kuwa mapenzi yake na Jux hayakuwa ya kisela kwani walikua wako na mapenzi ya dhati ingawa iliisha katikati.

“Mapenzi yangu na Juma hayakuwa ya Kisela, lakini pia sitaki na ninakemea kwa nguvu mapenzi ya kisela. Kuhusu kuimba wimbo huu nikwamba nimewasaidia wanawake wenzangu ambao huwa wanaingia kwenye mahusiano bila kujua ni mahusiano ya aina gani waliyonayo. Lakini kwenye uhalisia mimi siishi maisha hayo,” Vanessa aliambia EATV.

Tazama wimbo wa Vanessa Mdee ‘Kisela’ hapo chini:

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere