Vanessa Mdee na Ndoto Yake Ya Kusambaza Viatu Vyake Afrika
Staa wa muziki wa Bongo fleva nchini Vanessa Mdee ‘Vee Money’ ameibuka na kuweka wazi kuwa Hivi sasa Ndoto Yake kubwa ni kuviona viatu vyake vinasambaa Afrika nzima.
Vanessa ambaye hivi karibuni alizindua bidhaaya viatu vyake vya kike hususani kwa wanafunzi, amesema yupo kwenye mchakato wakuvisambaza Afrika nzima.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Dimba, Vanessa Mdee amesema kuwa moja ya mikakati ya kupanua soko la bidhaa za viatu vyake ni kuviuza nje ya Tanzania.
Nategemea brand yangu kuipanua zaidi na ili ikue nategemea kupata masoko katoka nchi mbalimbali za Afrika, lengo ni kuwafikia wanafunzi wengi wa shule za kiafrika“.
Viatu hivyo vinapatikana katika maduka mbali mbali nchini Tanzania na vinafanya vizuri kwenye mauzo yake sokoni.