Vannesa Asema Haamini Show Arusha Kufanyika, Ilikuwa Ikipigwa Vita.
Mwanadada Vanesa Mdee amefunguka na kusema kuwa hakuamini mpaka kufanyoka kwa show yake ya in love and money katika mkoa wa Arusha kutokana na ukweli kuwa show hiyo ilikuwa ikipigwa vita sana tangu hapo mwanzoni,
Vanesaa amabe kwa sasa yuko katika tour na mpenzi wake Jux kwa ajili ya mshabiki na wameshazunguka baadhi ya mikoa zaidi ya mitano anasema kuwa ilikuwa ngumu kukamilisha show hiyo kutokana na ukweli kuwa kulikuwa na watu waliotaka isifanikiwe.
akiandika katika ukurasa wake wa instagram na twitter, vanesa anasema “nipo hapa leo kwa sababu ya kumtumainia mungu, na kumuamini yeye , maana hii show ya arusha ndugu zangu ilikuwa inapigwa vita zaidi ya kawaida.nikisema kwamba asubui ya jana yaani siku ya show nilikuwa nilishajiandaa kurudi Dar, sababu mambo yalikwama , would you believe me? lakini mungu ana malaika wake anaopigana na wanyonge .Let me start by thanking my home town Arusha.”