Vannesa Mdee Aamua Kujipongeza Mwenyewe.
Mwanadada Vanesa Mdee amechoka kuvumilia na kusubiri sifa kutoka kwa watu wengine na kuamua kujipongeza mwenyewe kwa jitihada kubwa ambazo amekuwa akizinyesha na kupenyeza muziki wake kimataifa zaidi,
Vannesa anasema kuwa anajipongeza mwenyewe kwa sababu yeye ndie msanii pekee aArika Mashariki lakini msichana pekee wa Afrika kusaini deal kubwa Duniani lenye utafauti na madeal yote waliyowahi kusainiwa na wasanii mbalimbali.
Najipongeza mwenyewe kuwa msanii pekee wa kike tanzania actually msanii pekee wa Tanzania na East Afrika kupata deal kubwa na yenye utofauti na wengine .Ninafuraha sana kukutana na ma-director wakubwa wa Universal , pamoja na kutumbuiza katika ufunguzi wa afroforce …hii sio ndogo kwangu na hata kwa mashabiki zangu pamoja na watanzania kwa ujumla.
Wikiend hii zilisambaa picha nyingi za vannesa zikimuonyesha akiwa jukwaani ambapo alikuwa moja kati ya wasanii wakubwa walioimba katika tamasha la uzinduzi wa afro force