Vj Penny Afungukia Tuhuma Za Kutoa Mimba Ya Diamond Wakati Wapenzi

Mtangazaji na Vj maarufu bongo Vj Penny amefunguka kuhusiana na tuhuma zinazomkabili za kutoa mimba ya aliyekuwa mpenzi wake Mwanamuziki Diamond Platnumz.

Siku chache zilizopita  Diamond aliachia ngoma zake mbili mpya ‘Sikomi’ na ‘Niache’ ambazo zilizua gumzo kwani kwenye nyimbo hiyo amezungumzia kuhusu wapenzi wake wa zamani ambao ni Wema, Penny, Zari, Hamisa.

download latest music    

Penny na Diamond walikuwa na uhusiano wa kimapenzi miaka minne iliyopita lakini waliishia kuachana baada ya picha za Diamond na Wema kusambaa mtandaoni wakiwa pamoja.

Wakati Diamond na Penny wakiwa kwenye uhusiano habari zilisambaa kuwa Penny alibeba ujauzito wa Diamond lakini baadae ghafla mimba ile haikuonekana tena na baadae Penny mwenyewe alikana taarifa hizo na kudai kuwa hakubeba mimba ya Diamond.

Kupitia wimbo wake wa ‘Sikomi’ Diamond ameongelea penzi lake na mrembo Penny na kudai kuwa Penny alibeba mimba yake taarifa alizozifurahia akamgharamia mahitaji yake yote ikiwemo kumnunulia gari lakini akaitoa mimba yake.

Penny aliulizwa kuhusu tuhuma hizi za kutoa mimba ya Diamond na Dizzim online na akafunguka yafuatayo:

Kwanza naomba nimpongeze kwa nzuri aliyoifanya halafu suala la kutoa mimba yake ni la siku nyingi yaani la muda mrefu ambalo limekuwa likizungumzwa yaani tangu zamani linaongelewa tu lakini Kama yeye mwenyewe aliona ni sawa kulikumbushia basi hakuna ubaya”.

Baada ya kutoa nyimbo hizi ambazo zinafanya vizuri kwa hivi sasa mashabiki wengi walimjia juu Diamond na kudai kuwa wanachoshwa na vitendo vya Diamond kuimba ma-ex zake kwenye kila nyimbo zake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.