Warembo Wa Bongo Movie Wataja Siri Za Bata Za Dubai

Wasanii wanaosumbua katika tasnia ya Bongo movie warembo Aunty Ezekiel na Halima Yahaya maarufu kama Davina wamefunguka na kuanika Siri ya wao kula bata ndefu nchini Dubai.

Davina ameweka wazi kuwa siri kubwa ya wao kuweza kujihudumia na kula bata ndefu Dubai ni Faida za vikoba ambavyo wamekuwa wakijiwekea akiba kwa muda mrefu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Mtandao wa Global Publishers, Davina  alisema watu wasishtuke sana kwa bata hizo kwani Vikoba vyao vina mpango wa kuwapeleka wanachama wake sehemu mbalimbali duniani hivyo wao bata lao wamekwenda kulila Dubai.

Unajua watu wakituona tunakula bata kama hizi wanakimbilia kudhani tumewezeshwa na wanaume, hapana! Na hii naipigia mstari kwa sababu naujua ukweli, sisi tunawezeshwa na mfuko wetu wa Vikoba ambao una maendeleo makubwa na kwa mwaka huu watu wategemee makubwa kwani tuna filamu ambayo tutaicheza pia”.

Wasanii hao wametaja siri yao hiyo kutokana na tetesi zilizosambaa kwenye Mitandao ya kijamii kuwa kuna pedeshee mmoja ambaye amesimamia kuona warembo hao wanakula maisha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.