Wasanii Hawakumtumia Mzee Ipasavyo:-JB

Msanii wa bongo movie jacob steven amefunguka na kusema kuwa wasanii wengi hawakumtumia Mzee Majuto ipasavyo kipenzi cha uzim wake hivyo hawakuachiwa urithi mwingi wa jinsi ya kufanya kazi kama alivyokuwa yeye mwenyewe.

Akiongea na waandishi alipokuwa katika viwanja vya Karimjee jijin Dar katika shughuli za kuaga mwili wa marehemu kabla haujasafirishwa kwenda tanga, JB anasema kuwa pamoja na kwamba hata yeye aliweza kucheza nae filamu mbili, ya shikamo baba na nakwenda kwa mwanangu lakini bado anaona kuwa bado kuna vitu vingi bado hawajajifunza kutoka kwao.

download latest music    

Jb anasema kuwa Mzee alikuwa mtu wa pekee na ndio maana hata kazi zake zimekuwa haaizchoshi machoni pa watu na zimekuwa zikipenda pamoja na kwamba zilikuwa za zamani na zimekaa katika soko kwa muda mrefu.

Mzee Majuto alitufundisha kuwa  tukithamini na kuheshimu kazi za filamu , tunaweza kuwa na mafanikio mengi kuliko tunavyofikiria. na tutaacha kulalamika kwa sababu vitu vingi anavyovimiliki vilikuwa vinatokana na sanaa yake.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.