WCB Watangaza Mdhamini Wa Wasafi Festival, Ali Kiba Atupwa Kule

Msanii wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ametangaza kinywaji rasmi kitakacho dhamini Tamasha la Wasafi Festival linalotegemewa kuanza tarehe 24 November.

Mpaka siku ya jana ilikuwa inaaminika kwamba Ali Kiba kupitia kinywaji chake cha Mo Faya ndio watakuwa wadhamini rasmi wa Wasafi Festival hii ni Baada ya Diamond kukubali mwaliko wa Ali Kiba kudhamini tamasha hilo.

download latest music    

Siku mbili zilizopita Diamond alitangaza kuwa kinywaji Fulani ndio kitadhimini kinywaji hiko ambapo kupitia ukurasa wake wa Twitter aliandika:

Management imenambia kuna Kinywaji kesho kinaingia Rasmi onboard kama Mdhamini Mkuu wa #WasafiFestival2018 …Labda nikitaarifu tu kuwa kijiandae kutengeneza Storck za kutosha maana sio tu kunywewa, bali hata wengine watataka kukiogea kwa promo ntayokipa…. “.

Lakini jambo hilo limekuwa tofauti kwani usiku wa jana Diamond ametangaza kuwa kinywaji rasmi kutakacho dhamini Tamasha la Wasafi Festival ni Pepsi ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika:

https://www.instagram.com/p/BqNo1pehxso/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=irbye9kwk5xm

Mpaka sasa bado haijajulikana Kama Ali Kiba Kupitia Mo Faya bado atadhamini tamasha hilo au ndio basi katupwa kule lakini hawajatoa mrejesho wowote.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.