Wema Sepetu Aendelea Kukwepa Habari Za Kukatwa Utumbo

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu alijikuta katika wakati mgumu mapema wiki hii baada waandisha wa habari kumbana kuhusu taarifa zake za kukatwa utumbo nchini india.

Baada ya Wema kushindwa kufika mahakamani  chache zilizopita kuna taarifa zilienea kuwa Wema alienda India kwa ajili ya kukatwa utumbo ili apunguze unene aliokuwa.

download latest music    

Lakini tangu mwanzoni Wema amekuwa akikataa taarifa hizo na kudai yeye ni mzima lakini alikiri kiwa alienda India kwa ajili ya matibabu kutokana na ugonjwa mwingine ambao hajauweka wazi.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Wema alikubali kuwa alikuwa anaumwa lakini aligoma kuweka wazi alikuwa anaumwa ugonjwa gani hasa:

Ni kweli hapa katikati nilikuwa anaumwa lakani namshukuru Mungu nimepona. Siwezi kuzungumzia nilikuwa naumwa nini hiyo ni privacy yangu, sasa kama video mliiona ndio ni kweli nilikuwa naumwa lakini kuhusu ugonjwa hapana”.

Habari ya Wema kukatwa utumbo ili kupunguza mwili ilipamba moto Wikiend iliyopita baada ya kuonekana akiwa amepunguza kilo za kutosha tu Kwenye mashindano ya Miss Morogoro.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.