Wema Sepetu na Diamond Platnumz Wang’ara Tuzo Za Kimataifa

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu wamezidi kuipeperusha Bendera ya taifa baada ya kuchaguliwa kuwania tuzo za IARA Awards.

Wema Sepetu ambaye tayari ni Muigizaji bora wa kike katika tuzo za SZIFF amefanikiwa kuchaguliwa kuwania tuzo za International Achievement Recognition Awards (IARA) Kupitia Movie yake ya Heaven Sent.

download latest music    

Wema amechagulia kushindana katika kipengele cha Best International Actress huku akichuana na wasanii wengine wanne kutoka Africa ambao ni Joselyn Dumas kutoka Ghana, Amal Bouchoucha kutoka Algeria, Omotola Jalade kutoka Nigeria, Pearl Thusi kutoka South Africa na Tatiana Manslay kutoka Canada.

Kupitia page yake ya instagram Wema ameshukuru kwa kuweza kupata nafasi hiyo na kuwapa ujumbe mashabiki zake waendelee kumpigia kura kwa wingi  ili aweze kubeba tuzo hiyo:

And We are Nominated again…. Heaven Sent is still going places my loves…let’s keep on voting nawapenda nawajua Kwenye sekta ya kupiga kura tupo vizuri, tuseme INshalllah”.

Lakini pia Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amekuwa nominated katika kipengele cha Best Male  International Artist huku akiwa anachuana na wasanii kama vile Davido, MOhamed Abbas, LA Foune, Mr. P, Medikal, Black Coffee pamoja na Casper nyovest.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.