Zari Ajibu Mapigo Baada ya Sakata la Jana

Baada ya Msanii wa kizazi kipya Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ kukiri kuzaa mtoto na mwanamitindo Hamisa Mobetto, hatimaye mama watoto wake Zarinah Hassan azidi kumuweka njia panda juu ya uhusiano wao.

Mwanamama huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, ameeleza kupokea ushauri uliotolewa na baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii. “Watu wakiamua kuchepuka au kudanganya ni sawa na kujipotezea muda, ingawa wanahisi wanakuchezea wewe, hivyo usikate tamaa na kujilaumu wewe kwa ajili ya makosa ya watu wengine, maisha lazima yaendelee.

download latest music    

“Mambo yaliyotokea hayawezi kunipungizia hadhi yangu, usijilaumu kwa mambo yaliyotokea, zingatia malengo yako na kufanya maisha yako yaendelee”.am edema Zari.

Amesema kuwa yale yote yaliyosemwa katika sakata hili yanabaki yalivyo na muda huu anaamua kuyaweka kando na kuelekeza nguvu zake katika kusheherekea siku yake ya kuzaliwa.

Sakata hili limeibuka siku moja baada ya ya Zari kujibu mapigo katika mtandao wa Snapchat akionya asihusishwe na kitendo alichokifanya Diamond, cha kuzaa na Hamisa Mobetto.

Awali Katika maelezo yake mwanamuziki Diamond alisema kuwa ameshazungumza na mpenzi wake huyo kuhusiana na  mtoto aliyezaa na Hamisa na kwamba ameelewa na  hakuna tatizo tena.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.