Zari Ampiga Kufuli Diamond na Familia Yake

Mfanyabiashara maarufuu na mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari’  amedaiwa kuingia kufuli familia nzima ya Diamond.

Gazeti la Ijumaa linaripoti kuwa, Zari alianza kukata mawasiliano na Diamond, lakini alikuwa akiendelea kuwasiliana na ‘mkwewe’, Sanura Kassim ‘Bi Sandra’ na wifi yake, Esma Khan kabla ya kuwa-block wote.

download latest music    

Unajua Zari ni mtu mwenye misimamo sana. Baada tu ya kutangaza kummwaga Mondi Februari 14, mwaka jana, alisema penzi lake na Mondi limekufa, lakini hawezi kukata mawasiliano na familia yake maana wao hawana makosa yoyote.

Ndiyo maana ulikuwa unaona akaunti ya mama Diamond anayotumia jina la mama Dangote kwenye Insta ilikuwa inaendelea kupendeza na picha za wajukuu zake, Tiffah na Nillan kwa sababu Zari alikuwa vizuri na mama Dangote (mama Diamond), lakini baadaye walivyoanza kumletea mapichapicha ya wanawake wengine, Zari akaona isiwe shida, acha awafyekelee mbali”.

Baada ya tetesi hizo kusambaa Gazeti lilimsaka Esma Platnumz  ambaye alikiri kupigwa block muda mrefu, lakini akasema haoni tatizo kwani hayo ni mambo yao binafsi, lakini zaidi ni kwamba wao wanamuunga mkono ndugu yao pale anapokuwa kwenye uhusiano wake.

Sisi hatuwezi kuingia sana kwenye uhusiano wa Nasibu (Mondi), lakini huwa tunamsapoti pale anapokuwa. Kwa sasa yupo na Tanasha, basi tunamuunga mkono“.

Siku za Hivi karibuni Zari ameonekana kuwa mbali na Familia ya Diamond na kuonekana akiwa bize na maisha yake na Watoto Wake nchini Afrika ya Kusini.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.