Billnas Afunguka Sababu Za Kumpotezea Nandy

Msanii wa Hip hop nchini William Lyimo maarufu kama BillNas amefunguka na kuweka wazi sababu zilizopelekea kumpotezea aliyekuwa Mpenzi Wake Faustina Charles ‘Nandy’ wikiend iliyopita.

Wikiendi iliyopita Msanii Nandy alifanya uzinduzi rasmi wa albamu yake ya ‘The African Princess’ na katika hafla hiyo Billnas alikuwepo ndipo Nandy alipomfuata Billnas kwa ajili ya kuimba wote lakini cha ajabu Billnas alimpotezea kabisa Nandy.

Baada ya sakata hilo BillNas amefunguka Kwenye mahojiano na kipindi cha Enews na kusema sio kila sehemu anaenda Kama msanii kuna sehemu nyingi anaenda Kama mtu wa kawaida tu na anakuwa hayuko tayari kuimba  na haikuwa lazima kushiriki kama msanii.

Sapoti niliyotoa ya kununua albamu na kufika pale ilitosha, sioni sababu ya kuendeleza uadui kati yangu Mimi na Nandy Mimi nilienda pale kumpa sapoti yangu ya kweli kama msanii mwenzangu na si vinginevyo, hivyo alivyonipa mic sikujuwa nifanye nini kwa muda ule kwa kuwa sikuwa tayari kuimba kabisa”.

Lakini pia Billnas amefunguka kuwa ni miezi Sita imepita tangu atoe nyimbo yake hivyo amewataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kwani muda wowote anaachia mambo.

Bill Nas Athibitisha Kuwa Yupo ‘Single’ Kwa Sasa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na hit single yake ya ‘Labda’ William Lymo maarufu kama Billnas ameweka wazi kuwa kwa sasa hana mpenzi yaani ni Single Boy.

Bill Nas amefunguka na kudai hivi sasa yupo single hana mwanamke Lakini pia kinacho mtatiza ni kwamba bado hajajua ni mwanamke gani ambaye anatakiwa kuwa naye Kwenye Mahusiano.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Star Showbiz, Bill Nas amesema kwamba hahitaji kukurupuka, anachotamani ni kupata mtu sahihi ili aweze hata kufunga naye ndoa na si kuwa kwenye uhusiano ambao unaanza leo na kumalizika kesho.

Watu wanaweza wasiamini lakini ukweli ni kwamba kwa sasa sina uhusiano wa aina yoyote ile. Kinachonikwamisha kuingia ni kwamba sioni bado mwanamke sahihi wa mimi kuwa naye.

Ninasubiri pengine Mungu anionyeshe, huyo nitakayempata ndiye atakuwa mke wangu na sihitaji uhusiano wa kuanza leo na kuvunjika kesho”.

Bill Nas alishawahi kuwa Kwenye Mahusiano na msanii mwenzake Faustina Charles maarufu kama Nandy lakini wawili hao waliachana siku za nyuma kidogo.

Bill Nas Adai Kuwa Video Ya Ngono Na Nandy Haikuathiri Mahusiano Yake

Staa wa muziki wa Bongo fleva Bill Nas amefunguka na kusema pamoja na kwamba video yake ya ngono na Nandy ilivuja lakini mahusiano yake hayajavunjika.

Miezi michache iliyopita Bill Nas na Nandy walikumbwa na masahibu mazito baada ya video yao ikiyowaonyesha wakiwa faragha kuvuja Kwenye mitandao ya kijamii.

Lakini Bill Nas anaiambia Bongo 5 kuwa pamoja na video hiyo chafu kuvuja na kuonekana na dunia nzima mpenzi wake hakumuacha bali alizidi kuwa katibu naye katika kipindi hiko:

Hapana sijaaachana na mpenzi wangu nipo naye hadi sasa na ndio mtu pekee nilikuwa nawasiliana naye kila saa. She is very clever anajielewa, alitazama kwanza, alijua, akaangalia ni kwa namna gani anaweza kujenga kuliko kuharibu zaidi”.

Lakini na kwa upande wa Nandy pia Hivi karibuni akiwa katika media tour nchini Kenya alisema kuwa Boyfriend wake amemkataza kuzungumzia suala hilo ila bado penzi lao linaendelea na hali kuvunjika kwa skendo ile.

Nandy na Billnas pia wamesisitiza kuwa wameendelea kuoa marafiki na kuweka skendo ile nyuma.