Shamsa Ford afunguka kuhusu skendo ya ujauzito

Msanii wa Bongo Movies, mrembo na ambae anafanya vizuri katika tasnia hii ya filamu  kwa muda mrefu ,mwanadada Shamsa Ford amefunguka na kusema ukweli kuhusu tetesi zinazizidi kusambaa mitandaoni kuhusu yeye kuwa mjamzito , Shamsa ambae  amefunga ndoa hivi karibuni ikiwa ni kama  mwaka tu umepita  tangu ndoa yao na mumuwe   Chid Mapenzi  ameamua kusema ukweli  na kukanusha kuhusu tetesi hizo,Shamsa amekanusha kabisa taarifa izo na kusema kuwa hayo ni maneno ya watu tu katika mitandao wakitaka kumzushia kuhusu taarifa hizo.

“am not pregnant, mimi kweli kabisa sina  mimba” aliongea Shamsa  huku akicheka.

Kwa muda sasa kumekuwa na  tetesi mitandaoni huku watu wakisema kuwa Shamsa  ni mjamzito ,lakini Shamsa anakataa na kusema kuwa labda kwa sababu amekuwa akionekana mnene sana kwa muda sasa ndio maana watu wameanza kuhisi kuwa yeye ni mjazito,lakini unene wake ni kwasababu amejiachia na kula sana.

Hata hivyo Shamsa anaongezea kuwa inawezekana watu wanashawishika kuwa yeye ni mjamzito kutokana na picha zake alizopost hivi karibuni ambapo moja inamuonyesha amevimba uso kidogo na huku nyingine ikimuonesha akiwa  na mtoto wake wa kwanza wa kiume ikiwa na caption ya kusema anatamani kupata mtoto mwingine maana huyo aliyenae ameshakuwa.

Shamsa anaongezea kwa kusema kuwa watu wengi wamezoea kuwa mtu akishaolewa basi kinachofuata ni mimba na mtoto,lakini kwa upande wao bado hawajapanga kuzaa kwa sasa bado wanatafuta maisha mungu akujalia basi watapata mtoto “mimba ni jambo la kheri,kwanini nifiche,..nikipata basi Inshallah ”

Alipoendelea kuulizwa na mtangazaji wa kipindi cha eNews cha EATV ,kwamba kwanini watu wanasema wanamuona hadi anaenda kliniki Shamsa anasema hajawahi kwenda kliniki na ikitokea amepata mimba hawezi kufika  na kwasababu mimba inakuwa basi tumbo haliwezi kufichika.

Shamsa ameolewa ni mwaka mmoja  umepita tangu akiwa amefunga ndoa yake na kwa sasa anamtoto mmoja wa kiume anaeitwa Terry, na kama kweli Shamsa ni mjamzito basi tunamtakia afya njema yeye na mtoto wake.

Aunt Ezekiel aeleza sababu zake za kutotokea kwenye Bongo Movies

Aunt Ezekiel ambaye ni muigizaji wa movie za Bongo hivi karibuni amefunguka kueleza mbona haonekani kwenye movie hizi Kama kitambo.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Mrembo huyo ambaye ni mama ya mtoto mmoja na mpenzi wa dancer kutoka Wasafi Records hivi karibuni alifunguka kudai kuwa anapumzika kwa sasa lakini hivi karibuni. Aunt Ezekiel alikiambia kipindi cha Twenzetu cha Times FM.

“Bongo Movie tunaweza kusema ni kama maisha ya binadamu, kuna time analala, anaamka, anapika, so kunakuwa na kazi tofauti tofauti. Naweza kusema kwa sasa hivi Bongo Movie ni muda wetu wa kurelax kwanza kwa hiyo tumepumzika, tumelala tukishaamka nadhani tutakuja na vitu vingi vya tofauti.”

Aliongeza,

“Sio kwamba tukilala ndio hakuna kitu ambacho kitakuja kikubwa zaidi au hakitachukua akili za Watanzania tena, hapana kulala kwa Bongo Movie ni kulala kwa kujipanga ili tunapokuja kurudi tena turudi vizuri, so mimi siamini kama Bongo Movie imekufa, tumerelax tu,”

Hata hivyo aliyekuwa rafiki yake wa karibu Wema Sepetu amekuwa akiachia projects zake mpya pole pole.