Dude Awatolea Povu Wanaomponda Rais

Msanii wa bongo movies Kulwa Kikumba amefunguka na kuwakanya wale wote ambao wamekuwa na tabia ya kumsema vibaya Mh Rais kutokana na jitihada anazozifanya huku wakisema kuwa hakuna jipya na la maana.

Msanii huyo ameyasema hayo leo alipokuwa katika moja ya safari waliopangiwa na Mh mkuu wa mkoa , baada ya wasanii hawa kupewa ofa hiyo ya kutembelea miundombinu hasa ujenzi wa reli ya kisasa ya Morogoro hadi Dar Es Salaam.

Dude aasema kuwa kwa kile alichokiona kikiendelea hapo anaona kabisa juhudi kubwa za Mh Rais na amekuwa akiwashangaa sana wale ambao wamekuwa akisema kuwa mh hafanyi kazi yoyote.

Hata hivyo Dude ametoa wito kwa wasanii wote nchi kuwa mabalozi wa maendeleo na kutangaza mema ambayo Rais amekuwa akiyafanya kwa wananchi wake.

Dude pia ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha wasanii wote kuwa na umoja na  mshikamano kwa kila kitu hasa katika kufanya kazi na kuacha ubaguzi ambao mwisho wa siku hauna tija yoyote.

 

 

Dude Amwaga Povu Kwa Mashabiki Zake

Muigizaji wa Bongo movie Kulwa Kikumba maarufu kama Dude ameshindwa uvumilivu na kuamua kuwajibu mashabiki ambao wamekuwa wakimponda kwa Kitendo Cha kuposti picha akiwa anaswali.

SIku chache zilizopita Dude aliweka picha Kwenye ukurasa wake wa Instagram Ikiwa inamuonyesha akiwa anaswali jambo ambalo liliwakera mashabiki zake wengi.

Mashabiki walimjia juu Dude wakidai Dini hairuhusu mtu kujipiga picha ukiwa unafanya Ibadan halafu uje uweke Kwenye mitandao ya kijamii kwa nia ya kujionyesha.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers Dude amewajibu mashabiki kuwa alifanya hivyo ili kuwashawishi wengine kumcha Mungu.

Watu huwaona wasanii kama siyo wacha Mungu, kupiga picha nikifanya ibada kinawa­kumbusha wafuasi wangu wenye imani kama yangu ya Kiis­lamu kumkumbuka Allah”.

Dude sio msanii wa kwanza kukosolewa baada ya kuposti picha mitandaoni akiwa anasali kwani siku za nyuma Wastara alipata kichambo kama hiko baada ya kiposti picha akiwa anaswali.

Dude Ashauri Wasanii Wapewe Elimu

Muigizaji wa Bongo movie Kulwa Kikumba maarufu kama Dude ameitaka serikali iwasidie elimu wasanii ili waweze kuelimika katika masuala ya uwekezaji.

Dude amedai mambo ya wasanii kupata matatizo au inapotokea wanaugua wanakosa pesa za kutibiwa mpaka kufikia hatua ya kuchangiwa pesa na serikali ni la Kutia Aibu badala yake wapate elimu ya uwekezaji.

Kwenye mahojiano na Za Motomoto News Dude amesisitiza suala la wasanii kuugua na kushindwa kujilipia gharama za matibabu nje ya nchi limekuwa likimuumiza mno hivyo kuiomba Serikali kuwaboreshea mazingira ya kazi zao na kupatiwa elimu ya uwekezaji kwa hicho kidogo wanakichopata.

Tunaiomba Serikali ituboreshee mazingira ya kazi zetu maana tunateseka sana hasa pale tunapopatwa na magonjwa yanayohitaji matibabu ya nje ya nchi au hata hapa nchini. Pia tupate elimu ya uwekezaji kwa fedha hizi kidogo tunazopata maana hatuna elimu hiyo pamoja na bima ya afya”.

Siku chache zilizopita Msanii mkongwe wa Bongo movie Mzee Majuto alikosa kabisa pesa za matibabu mpaka kufikia hatua ya kuchangiwa na serikali ili akapate matibabu nchini India.