Nitafurahi Kama Diamond Atamuoa Wema: Esma Platnumz

Dada wa supastaa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Khan amefunguka na kudai kuwa atafurahi endapo kaka yake atamuoa Wema Sepetu.

Tangu Diamond atangaze kufunga ndia mwaka huu baada ya kuachana na mama watoto wake na mpenzi wake wa miaka mingi Zarinah Hassan ‘Zari’ swali pekee lililopo midomoni ni mwanamke gani ambaye Diamond anaweza kumuoa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na ‘Over the weekend’ alifunguka kuwa kwa upande wake hawezi kumchagulia mke kaka yake lakini Kama moyon wake ukiamua kurudi kwa Wema basi yeye moyoni mwake furaha zaidi.

Unajua Naseeb ndio anajua zaidi mke anayemfaa, lakini kama pia ataamua kurudi kwa Wema, mimi nitafurahi zaidi kwa sababu ni mtu ambaye tunapatana sana na ninampenda pia”.

Tangu Diamond atangaze ndoa kabla mwaka huu haujaisha kuna wanaodai atakayeolewa ni Wema wengine wanasema ni Zari na pia kuna wanaodai ni Hamisa.