Flora Mbasha na mumewe wa zamani wakorofishana tena

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Flora Mbasha na Emmanuel Mbasha waliachana miaka mitatu zilizopita lakini bado wako wakorofishana kwenye mtandao.

Emmanuel amemtupia maneno mke wake wa zamani baada ya kuzuka uvumi kuwa Flora alichapisha kitabu chake kinachoitwa ‘Siri za Flora Mbasha’ ambacho kinazungumia vitu mbaya kuhusu Emmanuel Mbasha.

Flora Mbasha na Emmanuel Mbasha

Ijumaa Wikienda lilimtafuta Emmanuel ambaye alionekana kuwa mwenye hasira kali alipoulizwa kuhusu kitabu cha mke wake wa zamani.

“Sipendi ujinga kwani watu hawawezi kuuza hicho kidaftari chao mpaka watafute kiki kwangu? Mbona wengine wanauza vyao kwa utaratibu mzuri? Mimi ninaingiaje kwenye ishu za huyo Flora? Zaidi ya miaka mitatu sipo naye na ni mke wa mtu, ninamuomba atulie na akome kunitajataja,” Emmanuel Mbasha alisema.

Kwa upande wa Flora alipotafutwa kuhusu ishu ya kumchafulia jina mume wake wa zamani, alisisitiza kuwa habari hizo za mtandaoni hazikuwa za kweli isipokuwa ni kweli kitabu chake hicho kimeshatoka na kinaelezea kiundani mambo aliyoyapitia kwenye ndoa yake na Mbasha kabla ya kuolewa na David Kusekwa.

 

 

Muimbaji wa nyimbo za injili Flora Mbasha alipata mtoto nje ya ndoa yake

Mume wa zamani wa muimbaji wa nyimbo za injili Flora Mbasha amedhibitisha kuwa msanii huyo alipata mtoto nje ya ndo kabla hawajaachana.

Emmanuel Mbasha na Flora Mbasha kabla hawajaachana

Emmanuel Mbasha alisema hayo akiongea na EATV siku ya Jumatano. Ishu hiyo imeibuka baada ya mmoja kati ya watu waliouliza maswali kumtaka Mbasha kueleza kuhusu mtoto wa pili wa Flora kama ni wake ama la.

Hapo awali Flora alikiri suala hilo wakiwa katika harakati za kuachana kwa mujibu wa sheria mahakamani, aliambia koti kuwa alizaa mtoto mmoja tu na mume wake Emmanuel.

Mtoto wao wa kwanza anayeitwa Elizabeth ndiye Flora alimzaa na mumewe wa kitambo, mtoto wa pili alimpata nje ya ndoa.

“Yule mtoto siyo wangu, hata katika hati ya mashitaka ya kuachanishwa na mahakama, yeye mwenyewe Flora kwa mkono wake akiwa na wanasheria wake, aliandika kwamba kwa kipindi chote ambacho aliishi na mimi alibahatika kupata mtoto mmoja pekee ambaye ni Eliza, kwahiyo mpaka hapo unajua kabisa kwa hapa imeshakula kwangu, ni kitu ambacho knauma sana, lakini kila mtu na ujasiri wake” alisema Emmanuel Mbasha.