“Akifuatilia ataumia kichwa” Gigy Money amjibu Mzee Majuto!

Gigy Money anaonekana mwanamke ambaye hamuogopi mtu yoyote. Mrembo huyu ambaye ni video vixen wa nyimbo za bongo hivi karibuni aliamua kumjibu Mzee Majuto ambaye alisema kuwa hapendezwi na picha zake za uchi mitandaoni.

Mzee Majuto

Kulingana na ripoti zinazoenea mitandaoni, Mzee Majuto anasemekana kuwa alidai kuwa picha za uchi hazipendezi kwa mwanamke na ndio maana hazipendi picha za Gigy.

Gigy Money
Gigy Money

Hata hivyo Gigy Money hivi karibuni aliamua kumjibu mkali huyu wa movie za bongo. Alisema;

“Kama hapendi swaga zangu ya nini asumbuke kutazama picha zan­gu. Hayo ndiyo maisha n­gu niliyo­chagua, akiyafua­tilia, ataumia kichwa bure, sioni cha ajabu kwangu kwa sababu kuna wasanii wengi tu wanakaa utupu,”

 

Baada ya kumchokora kwa muda Shilole hatimaye amjibu Gigy Money

Hapo awali Gigy Money alisema kuwa yeye sio shabiki wa Shilole wala nyimbo sake. Kulingana na mrembo huyu wa video za nyimbo za Bongo, shilole hajui kuzungumza kingereza vizuri na hii pia ndio maana hatamani kuwa shabiki wake!

Gigy Money

Hata hivyo, Shilole ameamua kumjibu mrembo huyu kupitia 5 Selekt ya EATV alipokuwa akifanyiwa mahojiano. Shilole alionekana kuto jali alichosema Gigy money na kwa sababu huyu ni Mudigi wake….hakuona haja ya kujibazana naye. Shilole alisema;

“Ni mdogo wangu kwa hiyo lazima apite kwa dada yake, kwa hiyo watu kama hao wadogo zangu ninawachukulia poa tu, hamna tatizo,”

Shilole aliendelea kwa kukiri kuwa ni kweli hajui kingereza lakini hilo sio jambo la kumsumbua akili;

“Kingereza is not my language, kwa hiyo nikisema bado hainilazimishi kukijua sana lakini najifunza kuongea, na pale panapobidi nitaongea. Hiyo ni kweli hamna shida kama sijaenda (shule) ni sawa, kwani watu wangapi hawajaenda shule, ukiwa umeenda shule na hela uwenayo.”