Harmorapa afunguka kuhusu uhusiano wake na Amber Lulu

Rappa kutoka Tanzania Hamorapa hivi karibuni kudai kuwa yeye na Amber Lulu wanatoka kimapenzi. Msanii huyu alikiri haya baada ya wengi kudhania kuwa uhusiano wao ni wa kiki.

Hii inakuja baada ya Lulu Diva kukana kuwa anauhusiano na Harmorapa. Hata hivyo rappa huyu ameiambia Boys Boys ya TV1 kuwa yeye kama mwanaume lazime awekatika mahusiano. Harmorapa alisema;

“Unajua siku zote kama ni mwanaume, halafu mwanaume rijali ni lazima uwe kwenye mahusiano ya kimapenzi, kwa hiyo mimi nina mpenzi, kuoa bado hata mtoto sina. Kwa sasa ni mtu famous, nilishamtaja ili kuna wengine hawamfahamu ni Amber Lulu,”

Hata hivyo hatujui ikiwa ni kweli hawa wawili ni wapenzi.

“Vanessa Mdee ananipa stress” Lulu Diva afunguka

Mwanamziki Lulu Diva ambaye anaonekana kutamba Afrika Mashariki kupitia wimbo wake Wa utamu amedai kuwa Vanessa Mdee ni mwanamke anayempa stress kila kukicha.

Vanessa Mdee

Mrembo huyu alisema haya katika mahojiano yake na Uwazi Showbiz. Kulingana na Lulu Diva, Vanessa Mdee ndiye ni mwanamziki ambaye ameweza kupenya kwenye muziki haraka huku akipata kollabo na wasanii wa kutoka inje – kitu ambacho wasanii wa kike bado hawajaweza kufanya. Lulu alisema:

“Bongo kwa wanamuziki wa kike kiukweli anayenipa stress ni Vee, kila mtu anafahamu kuwa ni mkali na anajituma kwenye muziki wake, sasa mimi malengo yangu ni kufanya kazi kwa juhudi ili kufika mbali, kwanza kuwa hapo alipo yeye na baadaye kupita zaidi,“

Hata hivyo Lulu Diva alisema kuwa anandoto za
kufanya muziki wa kimataifa siku moja.