Huyu ndiye mpenzi mpya wa Idris Sultan? (Picha)

Idris Sultan ameweka picha mpya ya mrembo ambaye hajukikani ni nani hata hivyo mchekeshaji huyu hakuwapa mashabiki wake nafasi ya kuwacha maoni yao baada yake kufunga comment section yake.

Hata hivyo hakuna anayejua ikiwa wawili hawa wanauhusiano ama ikiwa ni project yake mpya anayoitafutia kiki kwa kutowapa watu nafasi ya kuacha maoni yao.

Kwa sasa hatuna majibu ya maswali ambayo mashabiki wao wanauliza lakini imekuwa muda tangu Idris Sultan kuonekana na mrembo yeyote baada yake kuachana na Wema Sepetu. Hata hivyo kuna fununu mitandaoni kwamba wawili hao bado wanapendana lakini wameamua kuyaweka maisha yao kama Siri.

Tazama picha hiyo yake mpya hapa chino:

Ishara tosha Idris Sultan ni mkali wao katika Mitindo ya Fashion

Aliyekuwa mshindi wa Big Brother na mchekeshaji nchini, Idris Sultan ni mmoja wa Wanaume ambao wanajitambua katika Mitindo ya Fashion

Ingawa Idris Sultan siku hizi amekuwa kimya, picha zake huongea mengi kumhusu. Kupitia mtandao wake wa Instagram Idris Sultan huwaacha wengi wa kimmezea mate kwa sababu ya fashionable taste yake.

Ni mtu ambaye akivaa suti unatamani kumtazama mara kadhaa kwa sababu ni mtu ambaye huwa anapendeza. Kama huniamini tazama hizi picha Zake.

Kuna beef? Idris Sultan na Harmonize wachanana mitandaoni ya kijamii

Inaonekana kuwa Idris Sultan na Harmonize wameanza beef ambayo imewaacha mashabiki kama wameduwaa bila kujua ni yupi watampa support kwa kuwa wawili hawa ni mastaa wakubwa Bongo.

Kupitia mtandao wa Instagram, Idris Sultan alionekana akimtania Harmonize bila kujua kuwa muimbaji huyu hapendi mchezo. Idris aliandika kusema,

Ogopa rapa wako anapo kiki kuliko wewe. Inabidi mbadilishane wewe ndo uwe rapa.

Harmonize naye hakuchelewa kumjibu Idris Sultan huku akimchana kuwa anaskia kuwa amewekwa na mwanaume mwenzake na kuwa hakuwa na pesa anavyojigamba. Kupitia Twitter Harmonize aliandika kusema….

Nasikia unalala Mbezi kwa mwanaume mwenzio daa huruma. Kwani ulishindaga shilingi ngapi South…??? Mbaya zaidi nasikia unamarinda.

Idris naye kupitia Instagram alimjibu kwa kuposti picha hii na kuandika..

Idris Sultan

Acha nicheke tu, ntafanyaje sasa. Kumpiga nzi risasi ntamuonea maskini. Huyu ni makofi tu ??? #MarindaNimekuaSketiYaShule …. KARIBU KIUMENI ??

Chuki kubwa kati ya Idris Sultan na Harmonize na ni baada Sultan kutoa maoni mbovu kuhusu mziki wake

Uhusiano kati ya Harmonize and Idris Sultan uko mataani na ni baada ya Sultan kudiss mziki wake.

Jambo ambalo Harmonize alilizumgumzia kwenye Uheard by Clouds FM na Soudy Brown.

”Sina ushikaji na Idris, sina ushikaji naye na hatujawahi kukutana. Halafu kama sijawahi kukutania hata siku moja inakuwaje wewe unitanie?’

“Halafu nitanie vitu vingine ila usitanie muziki wangu. Tuheshimiane kila mtu aendelee kutafuta riziki yake na unaweza ukachekesha kuhusu vitu vingine na watu wakaelewa siyo lazima uchekeshe kwa kutania Brand ya mtu” – Harmonize alisema.