Joh Makini aeleza umuhimu wa kuachia audio kali badala ya kutumia hela mingi kwenye video

Imefika wakati ambapo Watanzania wameanza kurudi kisikiza audio badala ya kuangalia video za muziki kulingana na alichosema Joh Makini ambaye ni rapa mkali kutoka Tanzania.

Msanii huyu alisisitiza kuwa kuna umuhimu w kuachia audio kali atakama video yake haitakuwa imefika kiwango cha kuridhisha. Msanii huyu aliambia E-Newz ya EATV kuwa muziki ni audio na ikiwa mtu anapanga kufanya vizuri inabidi ajikaze kwenye mistari yake.

Msanii huyu alipeana mfano wa hapo zamani ambapo wasanii wengi hawakuwa wakitengeneza video kali ilhali audio zao zilikuwa zinafanya vyema, Joh alisema,

“Baadae ilipoanza mambo ya video ikawa hata mtu akitoa wimbo na video kali wimbo unakuwa mkubwa. Baadae Watanzania walipoacha kushangaa picha, imekuja wakati ukipiga video kali kama wimbo ni wa kawaida hautoki, kwa hiyo cycle ni ile ile, wimbo ni audio kwanza haijalishi video kubwa au ndogo kwa hiyo ngoma kama ni kali kwenye audio inafanya chochote.”

Baada ya mashabiki kumfananisha na Jay Z, Joh Makini asema haya

Wengi wanaopenda nyimbo za Bongo wananamtambua Joh Makini kama mmoja wa wasanii ambao wanapiga nyimbo ambazo zinapendwa na wengi Afrika Mashariki.

Joh Makini kwa kweli anatalanta ambayo imempa uwezo wa kufanya kazi na wasanii wakubwa kutoka Afrika na iwapo ataendelea hivyo miaka ijayo basi anaweza pia fanya kazi na wasanii kutoka nje ya Afrika.

Jay Z

Kwa sasa wengi wanamfananisha na rappa wa Marekani Jay Z, kitu ambacho kimemfanya kufurahi sana. Japo anajua kuwa bado anavitu vingi vya kufanya kabla kumfikia mkali huyu, Joh Makini amesema kuwa mashabiki wake kumuweka kiwango cha Jay Z ni kitu kubwa sana.

Akizungumza muimbaji huyo alisema,

“Jay Z ni ‘role model’ wangu…mimi naimba maisha ya sinoni daraja mbili na Tanzania na Jay Z anaimba maisha ya Brooklyn na Marekani, nafikiri nipo katika ‘level’ ambayo hawaoni mtu mwingine wa kunifananisha naye… Kwahiyo mimi naona poa kwa sababu kama unanifananisha na Jay z ‘yeah i like it’ kuliko ungenifananisha na mtu mwingine”