Monalisa Kuikabidhi Tuzo ya APA Bungeni

mwanadada Monalisa amabe ametua bongo siku ya jana kutokea nchin Ghana alipokwenda kwa ajili ya utaoji wa tuzo za african prestigious ambapo yeye pia ni mmoja kati ya walioshinda tuzo hizo kwa upande wa wanawake na Ray Kigosi kwa upand wa wanaume anatarajiwa kuipeleka tuzo hiyo bungeni siku za hii karibuni ikiwa ni kama nembo ya ushindi wa taifa.

Monalisa ambae pia alimpokelea rais wa Tanzania , tuzo hiyo na kuileta nyumbani baada ya Mh Magufuli kuchaguliwa kama kiongozi bora wa Africa, anatarajiwa kwenda bungeni kwa ajili ya kuipeleka tuzo hiyo.

Akiweka bayana hilo , mama wa msanii monalisa anaejulikana kama Mama Natasha amesema kuwa  baada ya monalisa kurudi kutoka Accra Ghana anatarajiwa kupokelewa jijini na kisa kwenda Dodoma kwa ajili ya kuipeleka tuzo hiyo Bungeni.

Hata hivyo katika ukurasa wake wa instagram, Monalisa amewshukuru watanzania wote kwa zaidi ya miaka 19 sasa tangu ameanza sanaa mpaka sasa wamekuwa nyuma yake na kusema kuwa hata tuzo aliyoipata ni kwa ajili ya wote na sio peke yake kwa sababu bila mashabiki wake isingewezekana.

 

Monalisa na Ray Kigosi Wang’aa Kwa Tuzo Nchini Ghana

Muigizaji wa Bongo movie Yvonne Cherry kwa Jina maarufu la usanii kama Monalisa ameng’aa kwenye tuzo za African Prestigious Awards (APA) zilizofanyika nchini Ghana.

Monalisa ameshinda tuzo kwenye kipengele cha Muigizaji bora wa kike nchini Africa. Tuzo hizo zilitolewa Siku mbili zilizopita.

Lakini pia Ray Vicent Kigosi pia ameibuka kidedea baada ya kukwapua tuzo ya Muigizaji bora wa kiume barani Africa huku wasanii kama Mzee majuto alibahatika kuchaguliwa kushindania Tuzo hizo.

Lakini pia Monalisa alipokea tuzo kwa niaba ya Raisi John Pombe Magufuli ambaye ameshinda tuzo kwenye kipengele cha Uongozi bora.

Kwa upande mwingine, Mtanzania Moise Hussein ameshinda tuzo hizo kwenye kipengele cha mpiga picha bora barani Afrika kwa mwaka 2017.

 

Monalisa Akabidhiwa Bendera Kupeperusha Nchi Ghana

Mwanadada Monalisa ambae ni msanii mkongwe sana katika tasnia ya filamu amekabidhiwa bendera ya taifa pamoja na ticket ya ndege na Mh  waziri wa michezo Harrison Mwakyembe kwa ajili ya safari yake ya kwenda Ghana ambapo ataenda kuepeperusha bendera ya Taifa katika maswala ya tasnia ya filamu kutokana na kuchaguliwa kwake katika kuwania tuzo za African Prestigious Award nchini humo .

Monalisa ambae alisindikizwa na mama yake  katika makabidhiano hayo katika ofisi za Baraza  walihudhuria pia watu mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Habari sanaa na Michezo Mh .Juliana Shonza pamoja na katibu mtendaji wa baraza la sanaa tanzania.

Monalisa anakwenda kuiwakilisha Tanzania baada ya kuchaguliwa katika kategoria hiyo na kuomba watanzania na afrika kwa ujumla kumpiagia kura kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa.Kila la kheri kwake.