Bill Nas: Sio Lazima Kila Mtu Ajue Mahusiano Yangu

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetamba kwa hivi sasa na ngoma yake ya ‘Tagi bovu’ amefunguka na kusema yeye sio msururu sana lakini anaona kuna baadhi ya vitu ambavyo anaona hamna umuhimu kuvianika na kila mtu ajue.

Bill Nas ametengeneza sana headlines kwenye mitandao ya kijamii wiki mbili tatu tangu atoke ngoma yake lakini kama kawaida kilichokuwa kinamfanya aongelewe sana ni mahusiano yake ya kimapenzi.

Kuna tetesi zilizosambaa toka mwaka jana na kudai kuwa Bill Nas ana Mahusiano ya kimapenzi na msanii mwenzake kutoka THT Nandy habari ambazo siku zote wawili hao wamezikataa na kusema wao ni marafiki.

Kwenye Interview aliyofanya na Dizzim Online, Bill Nas amekataa taarifa zilizodai kuwa yeye ni msiri sana hasa linapokuja suala la mahusiano yake na mpenzi wake ambapo Bill Nas amekiri hapendelei kuanika Mahusiano Yake hadharani:

Kusema ukweli mimi sio kwamba ni msiri sana ila hivi ndivyo nilivyo sio lazima kila kitu kila mtu ajue ama wafahamu kuna vitu watu wanapaswa kama binadamu waheshimu privacy yako na kuna vitu unatakiwa ubaki navyo mwenyewe au watu wako wa karibu”.

Bill Nas amekiri kuwa ana mpenzi wake lakini hayupo tayari kumuweka wazi kwa sasa na hizi skendo za yeye kutoka na wasanii wenzake zinakuwa kama zinamuharibia mapenzi yake.

 

Nandy Amkana Dogo Janja na Kumtamani Billinass

Msanii wa kike anaefanya vizuri katika tasnia ya muziki kwa sasa na wimbo wake wa kivuruge, Nandy  amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano na msanii Dogo janja kama vile watu ambavyo wamekuwa wakisema katika mitandao ya kijamii.

Kuna baadhi ya watu walikuwa wakisema kuwa kisa cha Nandy kuimba wimbo wa kivuruge ilikuwa ni meseji iliyotumwa kwa msanii Dogo janja baada ya kutemana nae na kwenda kutembea hadi kumuoa Irene uUwoya lakini Nandy amekanusha maneno hayo na kusema kuwa yeye na Dogo janja ni marafiki tu na hawana bifu lolote na wala hana uhusiano nae wowote hivyo hawezi kumuimbia wimbo huo.

Nandy amesema kuwa hajawahi kuwa na mahusiano na Dogo janja na wala hajawahi kumuwazia dogo janja labda wangemwambia kuhusu Billnasss kwa sababu ni msanii anaempenda sana na anatamani sana kuwa nae endapo msanii huyo atamfata na kuelezea hisia zake.

sijawahi kuwa na uhusiano na Dogo janja,ila ni mshikaji wangu tu na sijawahi kumfikiria  labda mngeniambi akuhusu Bilnass kwa sabau ni msanii wa kiume ninaempenda  na ninatamani siku moja awe wangu endapo atanifata lakini.-Alifunguka msanii Nandy.

miezi kadha nyumba nandy na billnass walisemekana kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na kusemekana kuwa walikuwa wakionwa sehemu mbalimbali, hata hivyo kwa upande wa billnass alishawahi kukuri kuwa Nandy ni msanii wa kike pekee ambae anaweza kuwaza kumuoa na anaeona kuwa ana sifa za kuwa mke.

Billnass na Nandy Wabanwa Pabaya

Wasanii wa Bongo fleva Nandy na Billnass wamejikuta katika wakati mgumu baada ya kubanwa na maswali kutokana na uhusiano wao.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi nying sana zilizotapakaa zinazodai ya kuwa mrembo Nandy au mwenyewe anavyopenda kujiita African Princess kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki anayefanya vizuri kwenye gemu na wimbo wake wa sina jambo. Tangu tetesi hizo zimeanza kutapakaa wawili hao kila mmoja kwa wakati wake wamejitahidi kuficha au kakataa kabisa kuhusiana kimapenzi na kudai kuwa wana urafiki tu wa kawaida ambao unaweza ukauita wa kikazi.

Jana kupitia stesheni ya Clouds Fm katika kipindi cha XXL kwenye segment ya U heard, Soudy Brown aliwavutia waya Nandy na Billnass kwa kutaka kuwahoji kwa kile kilichodaiwa kuna kiwanja walionekana pamoja ingawa kila mmoja aliweka picha kwenye mtandao wa kijamii akiwa peke yake (yaani hawakupiga wote picha) lakini picha hizo ziliwaonesha wakiwa katika eneo moja wakila bata. Soudy alivyomuuliza Billnass alijibu hivi;

Mimi sina ukaribu na Nandy wala sijawahi kutembea naye yaani kwa ufupi hayupo hata listi ya watu niliowahi kutoka nao. Sijawahi hata kumfikiria kutembea naye yaani sijui kitu chochote kuhusu Nandy yaani ukiniuliza kuhusu huyo mtu unakuwa unapotea’.

Baada ya kumuuliza Billnass na yeye kukana na kumruka futi 100 Nandy ikabidi tu ampigie na Nandy ili apate ukwdeli wake;

Unajua watu wanasema hivyo kwa sababu tulipiga picha kiwanja kimoja lakini sio ukweli mi nilienda na dada yangu na rafiki angu anaitwa Vai sina sababu ya kuficha kama ningekutana naye siningesema sina haja ya kuficha”.

Kila mmoja amesisitiza hatoki na mwenziye na kila mmja ni bachela lakini kama wanaendana fulani enhee??

Lakini anyway wazungu wanasema time will tell yaani muda ndo utasema alafu isitoshe mapenzi hayafichiki.