Nandy ataja baadhi ya changamoto anazozipata kwenye muziki

Nandy ni msanii ambaye ameanza kutamba Tanzania kwa haraka. Hata hivyo kama wasanii wengine pia yeye a spirit changamoto ambazo ameweza kuzitaja kwenye Interview yake hivi karibuni.

Muimbaji huyu amesema kuwa kwa sasa anajaribu kuwapa mashabiki wake nyimbo ambazo wasanii wengine hawafanyi. Kulingana na yeye inampaswa awe na ubunifu ambao utaweza kumfungulia njia za kupenya Afrika Mashariki.

Aliendelea kwa kusema kuwa changamoto anazopata kwa sasa ni kushindana na wasanii wa kike ambao wamepenya kwenye muziki. Akizungumza naTBC Taifa Nandy alisema,

Nandy
Nandy

“Yaani nikija kutoa wimbo usishuke au uwe juu zaidi, au nifanye ubunifu gani kutofautiana na wenzangu ili niweze kubakia katika nafasi yangu. Wasichana wote kwenye industry wapo katika ushindani  kwa sababu tunafanya biashara moja, kwa hiyo ninapomuangalia mtu kama Maua namuangalia kwa jicho la kama msanii mwenzangu, kwa jicho la kibiashara, kwa hiyo namuangalia kama mshindani wangu.”

Nandy adai wanaume wengi wamekuwa wakihaha kutaka kuonja penzi lake

Faustina Charles anaejulikana kama Nandy ni mwanamziki kutoka bongo na ukimuangalia, yeye ni msichana ambaye anawazingua wanaume wengi. Sio kwa rangi yake pekee lakini pia kwa sauti yake ambayo inaweza kumtoa nyoka pangoni.

Akiznungumza na Za Motomoto News, Nandy alikiri kuwa kwa sasa kuna wanaume kadhaa ambao wamekuwa wakimsumbua. Tangua kuachia wimbo na Chege – Nandy anasema kuwa hajapata amani ata hivyo hicho ni kitu ambacho wengi walitarajia kwani ni mrembo kupindukia.

Nandy
Nandy

Hata hivyo Nandy amesema kuwa hana mpango wa kuwataja wanaume hawa lakini wengi wao wanatamani sana kuonja penzi lake. Alisema,

“Usumbufu ni mkubwa mno kwa kweli, lakini siwezi kuwataja majina hata hao vigogo wanaonisumbua, mimi ni msichana ninayejielewa na wanaume wengi wamekuwa wakihaha kutaka kuonja penzi langu, wanagonga mwamba.”