Sababu ya kesi ya Masogange kutosikilizwa mwezi huu

Agnes Gerald anayetambulika kama Masogange bado anangoja kusikilizwa kwa kesi yake baada ya kutofika mahakamani Jana, Julai 13, 2017 kama ilivyohutajika.

Kulingana na wakili wa mrembo huyu, inasemekana kuwa hangeweza kufika kutoka na kuumwa kwa mwili. Wakili wake, Reuben Simwanza akizungumza na hakimu aliomba radhi kwa mteja wake.

Agnes Masogange
Agnes Masogange

Hata hivyo wakili wa Serikali, Constantine Kakula, hakufurahishwa na maneno haya huku akikumbusha mahakamani kuwa hapo mbeleni Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, alikuwa amepeana amri ya kuwa kesi hiyo ianze kusikilizwa Jana.

Agnes Masogange

Wakili wa Masogange aliweza kuisihi mahakama kuihairisha kesi kesi hiyo hadi July 25, 2017. Masogange hata hivyo ameshtakiwa kwa makosa ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroine na Oxazepam na Heroine.

Mahakama yatoa amri Agnes Masogange akamatwe tena

Video vixen wa bongo Agnes Gerald amejipata mashakani tena baada ya mahakama kutoa amri akamatwe kwa mara ya pili baada ya kutofika mahakamani kwa mara ya pili kesi.

Agnes ambaye hapo mbeleni alikosa kufika mahakamani wakati kesi yake ilikuwa ikitajwa amerudia kosa hili kwa mara ya pili baada ya kutofika mahakamani alipopangwa kutajiwa kesi yake.

Agnes
Agnes

Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam ametoa amri hiyo baada ya Masogange na wakili wake kukosa kuwasili. Kwa kosa hili sasa hivi Agnes Masogange atakamatwa kwa kutofika mahakamani na kutotoa taarifa ya kilichofanya kutofika.

Muigizaji huyu ana mashtaka mawili ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Agnes Masogange apewa onyo na Hakimu Mkuu baada ya kuchelewa kuwasili Mahakamani wakati unaotakiwa

Agnes Masogange ni mmoja wa Video vixen ambao wanajulikana sana Afrika Mashariki. Ameweza kufeature katika video kadhaa nchini Tanzania lakini hivi sasa yuko matatani na Mahakama baada ya kudaiwa kuwa mmoja wa watu maarafu anayetumia madawa ya kulevya.

Mwezi Februari aliweza kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo aliposomewa mashitaka yake kwa mara ya kwanza na kama wengi alikana na mahakama ikabidi kuhairisha kesi yake hadi, March 21, ili kuwapa polisi mda wa kutosha kufanya upelelezi wao.

Video vixen huyu anakabiliwa na mashitaka ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Hata hivyo Jumanne hii mrembo huyu hakuwa mahakamani kuskiza kesi yake baada ya kuchelewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilibidi kutaja kesi hiyo ingawa hakuwa.

Wakili wa Masogange, Nictogen Itege, aliweza kumtetea Masogange huku akisema kuwa yuko njiani. Masogange alipowasili Hakimu Mashauri alimtaka mshitakiwa kutii sheria anazopewa na Mahakama huku kesi yake ikihairishwa hadi Aprili 20, mwaka huu kwa kutajwa.