Aunty Ezekiel avunjika moyo baada ya ‘mama’ yake kufariki

Wikendi hii iliyopita mrembo wa filamu za bongo Aunty Ezekiel alimpoteza nyanya yake ambaye alimlea toka utotoni na kulingana na habari zinazoenea, bibi yake alikuwa kama mama na baba kwake baada ya wazazi wake kufariki.

Picha zinazoenea mitandaoni Aunty Ezekiel anaonekana kuwa na majonzi mengi lakini marafiki zake walikusanyika kumfriji huku wengi wakiandika ujumbe kupitia nguvu kumtia nguvu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Aunty Ezekiel aliandika kusema;

Kweli la mungu halina muhamuzi mungu akuweke mahari pema peponi bibi

Nandy afutilia mbali fununu kuwa amekosana na Dully Sykes

Nandy ambaye ni msanii mpya kutoka Bongo ameanza kuwapa wengi wasiwasi kwani anaonekana kuwa anatalanta ambayo itampa umaarufu Afrika Mashariki.

Hata hivyo hapo awali ilikuwa inasemakana kuwa Nandy na Dully Sykes hawakuwa wanasikizana lakini akizungumza hivi karibuni kupitia Planet Bongo ya EA Radio Nandy alisema,

Nandy
Nandy

“Yupo sana proud na mimi kila tukikutana huwa ananisisitiza kuwa na heshima, kusikiliza wakubwa walionitangulia, kufanya kazi kwa bidii kwa sababu hustling yangu aliiona toka way back na ndoto zangu anazijua nyingi sana,”

Aliendelea kwa kuzungumzia issue ambayo mashabiki wengi wanadai kuwa anajaribu kuwa Kama Ruby ingawa alisema,

“Kwa hiyo kaniambia ndoto zako zimetimia, so usiachia hiyo chance kwako kwa kufanya lolote baya.”

“Mimi simtaki Naseeb tena!” Wema Sepetu amwambia shabiki wake Instagram

Japo ni wengi bado hutarajia Wema Sepetu na Diamond Platnumz kurudiana, mrembo huyu ameweka wazi kuwa hamtamani Diamond tena na mapenzi yao yalikwisha kitambo sana.

Wema Sepetu alisema haya baada ya mmoja wa mashabiki wake aliandika kumuuliza iwapo ameshindwa kumpata Diamond Platnumz kupitia Instagram. Shabiki huyo aliandika kusema,

Wema Kwa uzuri huo umeshindwa kumkamata Diamond mpaka anakupa mawazo wanaume hawana lolote jitahidi

 

Kupitia tu Instagram Wema pia yeye alimpa shahidi huyo jibu ambalo lilidhibitisha kuwa mrembo huyu ameyaacha maisha yake ya kitambo na hivi sasa anatarajia mwanaume ambaye atamchukua alivyo. Wema aliandika kusema,

@Veronikakihonga Sasa baby alokwambia mi namtaka Diamond ni nani…?Life has to go on… Yule ni baba wa watoto wawili Jamani… Its about time u guys accept that me and Naseeb are no more. Mnachotakiwa ni kuniombua ni nipate mwanaume Bora na sio Bora mwanaume…Mwenye heshima zake tena ambaye hata haijulikani…Kajisemea dada angu @mangekimambi…mwenye hela miiingi

Skyner amchanwa na Nay baada ya kuposti picha ya binti yao

Skyner aliyekuwa mpenzi wa msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego, hivi karibuni aliamuaibisha baada ya kuweka picha ya binti yao mitandaoni huku akijisifu kwa uzuri wa mwanae.

Hata hivyo Nay wa Mitego hakukipata alichotarajia kutoka kwa Skyner ambaye alimchana kupitia Instagram huku akifunguka kuwa Nay hajakuwa baba kwa manae kwa miaka ilhali anawadanganya watu mitandaoni.

Ujumbe na Nay wa Mitego ulisema,

Skyner ambaye alikasirishwa na ujumbe huu aliandika ujumbe akimshangaa Nay ambaye anasemekana kuwa hataki kutoa huduma kwaajili ya mtoto. Aliandika kusema,

“Thats face you make when you see your ‘daddy jina’ anakufanyia promotions na kudanganya Watanzania kama Oooh my Twin sijui nanunua pisto, hata chupi unayovaa hajui thamani yake maskini. Nimevumilia sana it’s 5 Years now nimejiskia kutapika na nimetapikaa. Am done Mungu wa mbinguni nakuomba unijaalie maisha marefu uwezo nizidishie riziki….. uzima wa afya nikuleee mwanangu aje akuone baadae Inshallah umekuja kuwa Waziri wa nchi & Raisi wa nchi then alete pua yake”

Aliendelea kwa kusema…

“Endelea na drama zako ila please shobo na mwanangu sitaki…Please unapost picha za mtoto wangu za nini…shobo dundo zanini? Sitaki shobo na mwanangu koma kama ulivyo komaaa…Je, Wababa anaojisifu kama wanapenda watoto wao then hata hawajui mtoto anakula nini anasoma wapi anavaaa nini Wapooooooo? Drama nyingi sana mtandaoni halafu i love You Nyingi Hana Analofanya Wapooooooooo ??? Am done”

Aliendelea kwa kuonyesha binti yake alivyokuwa muhimu katika maisha yake alivyoandika kusema…

“Hakuna anayejua thamani yako zaidi yangu hata huyo anayejita baba’ko hana analolijua kuhusu wewe, si shule, malazi wala chakula kutwa kucha kukupost na kuongopea jamii kama anakujali, ninayehangaika nimie nakuhakikishia na kumuomba Mola wangu anijaalie uhai nguvu uwezo riziki nizidi kukulea kwa nguvu zangu Inshallah nakuonea gere sana umepata mama bora na sio bora mama uko mikono salama mwanangu wa uchungu. Happy Birthday My Happiness,” alisema Skyner.

Hata hivyo rapa huyo bado hajazungumza chochote kuhusu sakata hilo, Bongo5 bado inafanya jitihada za mtafuta.

‘Wengi walikushauri utoe mimba yangu lakini nakushuru kwa kunipa mtoto’ Rayvanny amwandikia mchumba wake ujumbe huu

Rayvanny na mchumba wake wamebarikiwa na mtoto wa kiume, Jaydan. Taarifa za kupata mtoto zilitolewa na Rayvanny kupitia Instagram.

Muimbaji huyu wa Wasafi alimpongeza mchumba wake kwa kumuandikia ujumbe ambao umeewacha wengi wakitamani mapenzi yao. Hata hivyo, Rayvanny aliweza kuweka wazi kuwa wengi walikuwa wakimsihi Fahyma kutoa mimba yake kwa sababu ya umri wake mdogo.

Lakini kwa sababu aliamua kuiweka na kuzaa Rayvanny amemfungulia roho kupitia instagram na kuandika kusema….

Rayvanny na mchumba wake
Rayvanny na mchumba wake

Kuna Kuachana, kugombana,kutengana lakini kuacha yote hayo Swala Kubwa Sana Ulilolifanya Ambalo sitoweza kulisahau ni Kunipa @jaydanvanny kwenye maisha yangu.Maana Ungweza Kutoa Mimba lakini Ulikua Na nia njema na mwanao .Wengi walikushauri Utoe wakasema unajiharibia Future wakasema bado mapema lakini haukua tayari kumpoteza Mwanao. @fahyma_ @jaydanvanny We love you son #Youngparents?

Huu ndio ujumbe Diamond Platnumz aliowaandikia watoto wake

Diamond Platnumz hivi karibuni aliwaandikia watoto wake ujumbe kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram kuwatania kwani wanamidomo ambayo inafanana na yake.

Hii sio mara ya kwanza kusikia muimbaji huyu akikiri kuwa wanae wanamfanana hasaa kwenye area ya mdomo. Na Kwa mara ya kwanza aliwaandikia ujumbe kuwasihi watumie midomo yao vizuri, kama alivyofanya yeye. Aliandika kusema,

Prince & Princess Lion!!!.. Midomo mkaitumie vizuri hiyo watoto….

Diamond aliambatanisha ujumbe huu na picha ya wawili hao kuonyesha wanavyofanana kisura. Kulingana na comments zilizoandikwa na mashabiki, wengi wao walipata wakati mgumu kuwatofautisha.

Hata hivyo ni kweli kuwa genes za Diamond na Zari zinatoa watoto warembo na picha hii aliyoipost inaonyesha kuwa ni ukweli.

Tiffah na Nillan
Tiffah na Nillan

Reality TV star wa Kenya Mishi Dorah adai kuwa Rayvanny alitaka kumpa mimba

Kilichotokea kati ya Mishi Dorah na Rayvanny hakiwezi julikana kwa kiukweli kwani wawili hao walikutana wakati ambapo hakuna yeyote alijua kuwa wana ‘mahusiano.’

Mishi Dorah

Hata hivyo, Rayvanny amekuwa akimkana mwanamke huyu kwa kusema kuwa anataka kumuharibia nyumba na jina lake. Lakini baada ya Ghafla kumhoji mwigizaji huyo wa Nairobi Diaries, Mishi Dorah alisema kuwa ni kweli aliweza kupatana na Rayvanny kimapenzi.

Mishi Dorah aliendelea kwa kusema kuwa hajapata hedhi zake kwa mwezi mmoja kuonyesha kuwa kunauwezekano wa mwanamke huyu kuwa na mimba ya Rayvanny kutokana na alivyosema. Kulingana na Mishi, Rayvanny alikuwa anataka sana wawili hao wapate mtoto wao wa kwanza kitu ambacho alihisi hawezi kuharikisha kwani hakutaka kuiharibu figure yake.

Lakini swali bado ni…Kati ya mwanamke huyu na Rayvanny nani anasema ukweli? Ebu itazame interview yake hapa.

https://youtu.be/wN6ppPh-TEI

Wema Sepetu amsifu Martin Kadinda katika ujumbe alioamwandikia kusheherekea siku yake ya kuzaliwa

Aliyekuwa manager wa Wema Sepetu, Martin Kadinda hivi leo amesherekea siku yake ya kuzaliwa na kama kawaida marafiki wake wa dhati wamekuwa wakimpost kwenye Instagram huku wakimsherekea leo.

Wema Sepetu ni mmoja wa marafiki waliompost Martin Kadinda. Katika ujumbe wake, Wema Sepetu alimsifu Martin na kumfungulia roho katika ujumbe wake uliowaacha mashabiki na tabasamu. Aliandika kusema,

Wema sepetu akiwa na Martin Kadinda

The World Knows How I feel about You… I have nothing more to add to dat… I love you more everyday than yesterday… (Mi nakupenda Leo kuliko Jana, ?) Happy Birthday wa kwangu mimi apa…. Wa Sunny, Wa Sunshine, Kaka manager wa kwanza kabisa duniani… Yaani hapa natafuta maneno mapya mapya ambayo sijawahi kukwambia ila najikuta nakosa maana yote nishamalizaga… Basi wacha niache kutype….

Wawili hawa wamekuwa marafiki kwa miaka mingi na ata baada ya Martin kuanza biashara zake, bado wako pamoja kama ndugu na dada.

Msanii mwingine kutoka kenya azuru WCB baada ya Willy Paul

Inaonekana kuwa Willy Paul sio msanii pekee kutoka Kenya ambaye anajulikana na Diamond Platnumz. Siku chache baada ya kuzuru Tanzanian kupromote wimbo wake I Do aliyomshirikisha mrembo kutoka Jamaica, Alaine… msanii mwingine anayejulikana kama Chikuzee kutoka pwani pia alikuwa kwenye ofisi za WCB hivi leo.

Msanii huyu anayejulikana sana pande za Mombasa Chikuzee aka Zee la Mavuvuzela ni alishare picha zake kupitia mitandao yake ya kijamii alipotembelea WCB.

Kwa hivi sasa kuna tetesi kuwa kuna kitu kiko jikoni baina yake na Rayvanny. Mashabiki wake kupitia kwa comments walitaka kujua kama alienda pale kutia sahihi mkataba wa kuwezesha ngoma zake kuwekwa kwenye wasafi.com ama kama walikuwa wanatengeza projects mpya.

Ata hivyo msanii huyu hajafunguka kueleza alikchokuwa akifanya ofisini mwa Diamond Platnumz lakini kuna uwezekano kuwa kuna jambo kubwa wawili hawa wanataka kuachia.

Msanii wa Bongo Fleva Linex adai kuwa kiki inaua muziki

Linex, msanii maarufu wa bongo amefunguka na kusema kuwa mtindo wa kupa mziki kiki unapoteza ladha na focus ya mziki nchini Tanzania.

Akiongea na waandishi wa global punlishers Tz nyumbani kwake Mbezi Beach Dar es Salaam, Linex amesema kuwa imekuwa kama trend ya wasanii wa Bongo kutokea na skendo wakati wanpotaka kuachilia mziki siku hizi. Kulingana na yeye vitendo kama hivi havina maana kama msanii anaamini kazi yake ni nzuri.

Msanii huyu aliendelea kusema kuwa mashabiki ndio wanaoamua kama projects za wasanii ni za kuvutia au la. Linex alisema,

“Nachoweza kusema turudi kushabikia muziki mzuri, tuache kushabikia skendo. Nachokiona hapa muziki unapotea kabisa”

Ata hivyo hit maker huyo wa Kiherehere aliwasihi mashabiki kuwa makini na kufuatilia muziki wa maana badala ya kushabikia skendo za watu maarufu.

“Naona amepanga kunichafua” Rayvanny amkana Mishi Dorah anayemdai kimapenzi

Rayvanny aliyekuwa nchini Kenya hivi majuzi amekana Mishi Dorah amabaye ni mwanake wa makamo na bado anamtaka Vanyny boy kimapenzi.

Staa huyu wa tanzanian amefunguka kwa kusema kuwa amekataa ofa za Mishi Dorah ambaye anaonekana kumharibia jina nchini Kenya na sasa pia Tanzania. Mishi ambaye ni mwigizaji wa reality show amekuwa akitangaza kuwa ashawai kuwa na Rayvanny kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, wiki iliyopita. Aliskika akisema,

“Ninampenda Rayvanny, nitamtafuta kwa udi na uvumba nimtunuku penzi ili roho yangu itulie, nampenda sana kwa kweli,”

Mishi Dorah

Ata hivyo Rayvanny sasa amefenguka huku akisema kuwa amekuwa akiona anachosema Mishi Dorah, lakini hatakai mambo ya mwanamke huyu kwani anahofia nyumba yake kuvunjika na pia brand yake kuharibika. Akizungumza Rayvanny alisema,

“Yaani sitaki kumuongelea kabisa huyo mwanamke, maana naona amepanga kunichafua kwani nilienda Kenya wakati f’lani nikakuta habari zake, huku nyumbani Bongo ndiyo hivi tena, sina cha kuongea maana mtu akiamua kukuchafua huwezi kuongea kitu.”

Mpenzi wa Rayvanny aonyesha tumbo lake likiwa uchi wiki kidhaa kabla ya kuzaa

Rayvanny na mpenzi wake fahyma wanamtarajia mtoto wao wa kwanza hivi karibuni kulingana na wanachoandika mitandaoni yao ya kijamii.

wawili hawa wanasemekana kuwa walianza mahusiano yao mwaka uliopita na kwa hivi sasa wanatajia familia yao kuongeza kwa sababu Fahyma ana mimba na kulingana na picha anazoziposti kwenye Instagram msichana huyu amebakisha wiki kadhaa kabla kuzaa mtoto wake wa kwanza.

Ingawa wawili hawa hujaribu kuweka mahusiano yao chini ya maji, Fahyma na rafiki wake wa Karibu ambaye alisemekana kuwa mpenzi wa Diamond Platnumz, Official Lynn, wameweza kushare picha mpya za Fahyma akioneshana tumbo lake huku kama amevaa overall ya kinyasa na crop top.

Mashabiki wa Fahyma walimsifu huku wakimpongeza kwa mtoto anayemtarajia hivi karibuni. Ikiwa bado hujaziona picha hizi basi ziangalie hapa chini.

Fahyma
Fahyma
Fahyma na rafiki yake official Lyyn
Fahyma na rafiki yake official Lyyn

Harmorapa awataja mastaa ambao waliompa jina analolitumia sasa

Rapper wa Tanzania, Harmorapa, kwa sasa hivi ni mmoja wa watu maarufu Afrika Mashariki. hii ni kwa sababu ya jina lake na pia nyimbo anazoziachilia.

Kabla ya kuwa staa mkubwa rapper huyo hakuwa anatumia jina hilo lakini baada ya kujitokeza na alikutana na mastaa kadhaa waliomshauri kutumia jina analotumia sasa.

Akizungumza katika show ya Bongo Dot Home cha Times FM, Harmorapper alisema kuwa Roma na Mr T-Touch ni watu ambao walimsihi kutumia jiona la Harmorapa na pia kwa sababu anafanana na mwimbaji wa Wasafi records, Harmonize

“Baadhi ya mastaa wakubwa katika muziki wa hapa Bongo nao walinishauri nijiite hivi, akiwemo brother Roma Mkatoliki na Mt T-Touch,”

Hapo mbeleni rapper huyu wa Tanzania alikuwa akifahamika kama Jembe la Kusini, jina ambalo ata mimi kama shabiki wake naona halingeweza kumake kwa hii industry.

“Wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,” Harmorapa ambia watu wanaomuongela vibaya

Staa na rapa wa Tanzania, Harmorapa hivi majuzi aliweza kufunguka kuhusu watu ambao wanamtusi na kumuongelea vibaya tangu awe maarufu.

Rapper huyo ambaye amekuwa akifanya vizuri Tanzania na Afrika Mashariki kupitia nyimbo zake hivi sasa ndiye anayepata kiki kubwa Bongo na anavyoonekana, Harmorapa atakuwa na umaarufu kama wa Diamond Platnumz iwapo ataendelea kurelease projects ambazo watu watapenda.

Hata hivyo, akizungumza na Bongo 5 rapa huyu alisema kuwa habebwi na kiki na kuwa kazi yake ndiyo inafanya awemaarufu kwa hivyo wanomchukia wanafanya kazi bure na kuwa ataendelea kuachilia nyimbo zake kama kawaida.

“Watu ambao wanahisi Harmorapa hatodumu kwenye game kwanza wanakosea halafu pia naweza nikasema kwamba wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,”

Aliendelea kwa kusema kuwa…

“Kama mimi binafsi nimejipanga sana vya kutosha. Unajua kwamba maneno yao mimi hayanivinjii chochote ni ile sawa na kumpiga chura teke na kumwongezea mwendo. Wanavyoniongea mimi ndo wananipa power na wananipa maujuzi na wananipa kuweza. Ni wao wananiweza mimi kuweza na kukaza ilmradi niweze kufanya kazi nzuri.”

Harmorapa  pia amehaidi mashabiki wake projects kubwa ambazo ataachilia mwaka huu.

Mtoto kapendeza! Zari Hassan amnyoa Nillan mara ya kwanza tangu azaliwe

Mtoto wa pili wa Zari Hassan na Diamond Platnumz , Prince Nillan ameachwa akifanana na babake baada ya kunyolewa na mama make hivi leo.

Kupitia mtandao wake wa Instagram Zari aliweza kupost picha hizi mpya za Nillan huku akimsifu alivyopendeza baada ya kumnyoa nywele zake.

Ni kweli kuwa Mtoto huyu ambaye ni mmoja wa mastar awachanga Tanzania anafanana sana na babake Chibu Dangote na Tiffah.

Wengi wa mashabiki wake wamekuwa wakimfananisha na dadake Tiffah na kusema ukweli hawa wawili wanakaa mapacha ingawa Tiffah atafikisha miaka miwili mwezi wa Agosti.

Ikiwa hujaziona picha mpya za Nillan, basi ziangalia hapa chini.

 

Agnes Masogange apewa onyo na Hakimu Mkuu baada ya kuchelewa kuwasili Mahakamani wakati unaotakiwa

Agnes Masogange ni mmoja wa Video vixen ambao wanajulikana sana Afrika Mashariki. Ameweza kufeature katika video kadhaa nchini Tanzania lakini hivi sasa yuko matatani na Mahakama baada ya kudaiwa kuwa mmoja wa watu maarafu anayetumia madawa ya kulevya.

Mwezi Februari aliweza kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo aliposomewa mashitaka yake kwa mara ya kwanza na kama wengi alikana na mahakama ikabidi kuhairisha kesi yake hadi, March 21, ili kuwapa polisi mda wa kutosha kufanya upelelezi wao.

Video vixen huyu anakabiliwa na mashitaka ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Hata hivyo Jumanne hii mrembo huyu hakuwa mahakamani kuskiza kesi yake baada ya kuchelewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilibidi kutaja kesi hiyo ingawa hakuwa.

Wakili wa Masogange, Nictogen Itege, aliweza kumtetea Masogange huku akisema kuwa yuko njiani. Masogange alipowasili Hakimu Mashauri alimtaka mshitakiwa kutii sheria anazopewa na Mahakama huku kesi yake ikihairishwa hadi Aprili 20, mwaka huu kwa kutajwa.