Mimi na Hemed Tumekuwa Tukigombana kila Baada ya Wiki Mbili :-Gelly

Msanii anaetamba kwa sasa na wimbo wake wa Washa amefunguka na kuongelea mahusiano yake na msanii mwenzake Hemed ambae anasema kuwa walikuwa watu wa kugombana sana kipindi cha nyuma lakini kitu cha ajabu ni kwamba kwa sasa hivi wamekuwa marafiki sana.

Gelly anasema kuwa hata katika baadhi ya kugombana kwao ilikuwa ni kwa sababu ya wanawake ambapo anasema kuwa hemedi alikuwa anweza kumzidi kete na akamchukulia mademu zake na hivyo yeye anachofanya pia ni kukaa vizuri na kujipanga na kumchukulia pia.

Mimi na Hemed tumekuwa tukigombana na kuzozana kila  baada ya wiki mbili,, tulishapigana sana lakini kwa sasa tumekuwa zaidi ya marafii yaani ni kama ndugu. Ananichukulia demu wangu na mimi nikikaa vizuri namchukulia wa kwake.

Kwa kumalizia katika mahojiano hayo Gelly anasema kuwa amekuwa mtu mwenye ndoto kubwa ya kutaka kuwa Producer wa filamu zenye mafanikio .

 

Hemed PHD ni Chawa Wangu- Gelly Wa Ryhmes

Mwanamuziki wa Bongo fleva Gelly wa Rhymes amefunguka na kudai kuwa msanii mwenzake wa Bongo fleva Hemed PHD pia ni chawa wake.

Hemed na Belly wamekuwa marafiki kwa zaidi ya miaka 11 wameshirikiana na kudhirikishana katika nyimbo zao mbali mbali lakini wameigiza pamoja filamu za bongo movie kadhaa na kwa nyakati tofauti wote wamesisisitiza kuwa wao kwa sasa ni zaidi ya marafiki wamekuwa kama ndugu kwa ukaribu wao.

Gelly amejibu fununu zilizopo mtandaoni zinazodai kuwa yeye ni chawa tu wa Hemed na hana mchongo mwingine wa maana hapa mjini, Gelly amesema yeye na Hemed ni zaidi ya ndugu hivyo watu wanaomuita chawa wake hawafahamu kuwa hata Hemed ni chawa kwake.

Gelly alifunguka hayo kwenye mahojiano na Enews ya EATV ambapo pia alizidi kuongeza:

Kwanza nilikuwa sielewi maana ya chawa mpaka uliponielezea kumbe chawa ni mtu ambaye yuko karibu na mtu basi kama ndio hivyo Hemed basi na yeye chawa wangu kwa sababu na yeye yupo karibu na mimi sana, anyway iko hivi mimi na Hemed sahivi tumevuka urafiki tuko kama brothers na ni watu tunaosaidiana kwenye kila kitu hata kutoa nyimbo lazima tushauriane kwaiyo tuko pamoja most of the time hasa hasa kikazi hata yeye akiwa na tatizo ananifuata ananiambia na mimi pia nafanya hivyo hivyo”.

Lakini pia Gelly ameongelea label yao pamoja naHemed inayoitwa Pappination lakini pia nyimbo yake aliyoitoa hivi karibuni inayoitwa ‘Vibenten’ ambayo ndani yake ameongelea vijana wa mjini ambao nivibenten lakini pia amedai amewataja kwa majina humo ndani.

Gelly Wa Ryhmes: Nilimgonga Demu Wa Hemedy PHD

Mwanamuziki wa Bongo fleva Gelly wa Ryhmes ametoa siri ambayo ilikuwepo kati yake na rafiki yake na mshkaji wake msanii wa Bongo fleva na Bongo movie Hemedy PHD ambaye amekiri kumchukulia demu wake.

Gelly wa Ryhmes alifunguka hayo alipokuwa anafanya mahojiano na LilOmmy ambapo alifunguka kuhusu historia ya urafiki wao na vikwazo ambavyo wamepitia kwa kutegemea wote wawili ni mastaa.

Hemedy PHD na Gelly wa Ryhmes

Gelly alifunguka yafuatayo kuhusiana na urafiki wake na Hemedy kwenye kipindi cha The Playlist;

Mimi na Hemedy tumekuwa wote Tanga shule tulizokuwa tunasoma zilikuwa karibu kwaiyo tulikuwa washkaji ambao tulikuwa tunaonana onana tu kwa juu juu lakini kila mtu alikuwa ana mishe zake lakini kilichofanya mpaka tukawa marafiki sana ni mwaka 2009 au 2008 nakumbuka ilikuwa shoo ya Ali Kiba iliyofanyika Zanzibar tulikutana kwenye boti njiani yaani from nowhere tukajikuta tunapiga stori alafu tumeendana wote tunafanya mziki basi tukawa washkaji kupitiliza mpaka sahivi tumeshavuka steji ya urafiki sahivi ni kama ndugu na ninavyokwambia tumepitia misala kibao tumekula goodtimes nyingi tumeshagombana sana always sisi hazipiti wiki mbili hatujazinguana lakini uzuri wetu mimi na Hemedy kati yetu hakunaga unafki mwenzako akikosea unamchana live”.

Lakini pia Gelly pia amefunguka kuhusu tetesi zinazosambaa kuwa yeye na Hemedy wanatabia ya kubadilishana mademu na hata kuna msala ulitokea kuwa Gelly alitembea na msichana wa Hemedy;

Stori yenyewe ilikuwa kwa kipindi kile nilikuwa sijatulia na demu wangu ambaye niko naye sahivi kwa kipindi kile kutokana na mambo ya ujana tu, lakini nakumbuka nilikuwa na msichana wangu nilikuwa namuelewa sana ile tunaanza mapenzi nikasikia Hemedy kamgonga nikimuuliza anakataa aisee ilikuwa bonge la ugomvi hadi Instagram huko watu walijua mwaka mzima hatukuongea kwaiyo na mimi nilichofanya ile tumekaribia kupata tu na mimi nikamgongea demu wake”.