“Wema Sepetu alitoweka” Haitham aeleza kwanini Wema Sepetu hakuonekana kwa wimbo wake ‘Playboy’

Haitham aligonga vichwa vya habari baada ya kutangazwa kuwa alimshirikisha Wema Sepetu kwenye wimbo wake mpya ‘Playboy’.

Lakini video ilipotolewa watu walipigwa na butwa kwani Wema Sepetu hakua kwenye video hio wala ata sauti yake haikusikika kokote.

https://www.youtube.com/watch?v=solY_OOnas0

Haitham sasa amefunguka kuhusu Wema Sepetu kutoonekana katika video yake. Akiongea na E-News ya EATV, mrembo huyo alisema Wema hakupatikana siku ambayo walikua wanashoot video yake.

Haitham hata hivyo hakueleza sababu zilizomfanya Wema Sepetu kushindwa kufika wakati walikua wanashoot video. Alisema kutoonekana kwa Wema katika video yake kulisababisha madhara kiasi.

“Na script ambayo tumefanya sasa inayoonekana kwenye video wasichana watatu ilibadilishwa fasta baada ya Wema kutokutokea kwenye video, so script ya mwanzo ambayo Wema alipaswa kuwepo aliandika yeye director na baada ya mabadiliko kutokea akabadilisha scrip. Kwa upande wingine yameathiri kidogo sio sana kwa sababu kuna baadhi ya mashabiki wa Wema walitamani kumuona kwenye video, kwa hiyo ameathiri kidogo kwa wale mashabiki walikuwa wanatamani kumuona,” amesisitiza, Haitham alisema.

 

Haitham aeleza faida ya kumshirikisha Wema Sepetu kwa wimbo wake – ‘Playboy’

Muimbaji Haitham alimshirikisha Wema Sepetu kwa wimbo wake mpya ‘Playboy’ ambayo alitoa siku mbili zilizopita.

Haitham amekiri kuwa amenufaika pakubwa na umaarufu wa Wema Sepetu. Akiongea na XXL ya Clouds FM, muimbaju huyo alisema kumshirikisha Wema kwa wimbo wake kumeongeza uzito wa jina lake.

“Toka nimetoa ngoma na Wema nimeona watu wamenipokea vizuri tena zaidi na zaidi lakini sio kwa sababu nimefanya na Wema pekee yake tu, kwa sababu ya muziki mzuri, watu pia wanasema muziki ni mzuri,” amesema Haitham.

Tazama wimbo wake hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=OCHVKnItJE0

Wema Sepetu ashirikishwa kwa wimbo mpya – ‘Playboy’ (Video)

Wema Sepetu ameshirikishwa kwa wimbo nyingine, Muigizaji huyo wa filamu za Bongo aliwai kushirikishwa na msanii Snura Majanga kwa wimbo unaoitwa ‘Shoga Yake Mama’.

Msanii Haitham kutoka Mj Records ametoa ngoma mpya inayoitwa ‘Playboy’ ambayo alimshirikisha Wema Sepetu. Mtayarishaji wa muziki kutoka Mj Records Daxo Chali aliambia Planet Bongo ya East Africa Radio kuwa alimtafuta Wema ili afanye kolabo na Haitham.

“Niliona wimbo wa Haitham unahitaji mtu nikafikiria nifanyaje, lakini wakati huo huo nilikuwa na mpango wa kuja kufanya wimbo ambao ningependa kuona Wema Sepetu anakuwepo, basi kwenye huu wimbo mpya wa ‘Play boy’ nikaona huyu humu atakaa. Nikaanza kumtafuta Wema Sepetu, kuna siku kweli akafika na kufanya. Wema Sepetu anajua sana kuimba watu wengi hawajui hilo, sema tu hizo ‘melody’ ndiyo zilimsumbua maana ni za kiswahili lakini zinaimbwa kama kifaransa lakini kwingine amenyoosha,” alisema Daxo.

Tazama wimbo huo – ‘Playboy’ hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=OCHVKnItJE0